Naja kwa jina lake Mungu Kwamba yalo moyoni mwangu Yaliyo tamu na machungu Uje kulimuka mwenzangu Ukituliana nikwambie Nitasema pasi kificha Nikuonye bila kukucha Kuwa jambo ‘kikufikicha La ukweli uliochacha Nihisani uniambie Hakuna aliyenyooka Muenda asiyeteguka Kwa wazo au kutamuka Miye pia wakupunguka Ukiona ila nambie Ni wa chira asoonyeka Muambae asokanyika Mara tatu hajaambika Atajuta akikutika Zamu yako ni umwambie kweli mchungu huuma Na hugharimu kuusema Ela ni dawa ya hatima Huja kuuponya mtima Ukiwa nao we’nambie Kanyo lako ukichelea Ukiniona nakosea Kwa Mungu ukijitetea Hesabu utanitolea Kujitoa ila,nambie Niambie liwapo chungu Usinifumbie mizungu Walau likawe uchengu Mwanga wa maozi yangu Usiche kuindha nambie
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!