Moyo wenye kupendao, tena haumilikiwi Hauwi wa apendao, wala maliye hauwi Humwendea apendwao, ukabakia kiziwi Moyo wenye kupendao, na subira hauwi Penzi huutiya mbio, ukawa katu hutuwi Kajikosa mmilikio, ‘kijaribu hatuliwi Kutuza kama atakao, hiariye haiwi Moyo wenye kupendao, na subira hauwi Huwashinda watu sao, una nguvuna kawi Ukawatoka ndanio, kwendeya ajinawi Ukawashinda nafsio, kawa haurudiwi Moyo wenye kupendao, na subira hauwi Ngajaribu wamilikio, kimiani hutiwi Unawatinga uchao, kichele hawatuliwi Penzi liupaniao, ni muzungu hujibiwi Moyo wenye kupendao,na subira hauwi Kama sivyo nisemao, mbona mja hambiwi, Akaziacha na mbio, kageuka ja kiziwi Akapuza waasao, na simile haambiwi Moyo wenye kupendao,na subira hauwi
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!