Nomba mkanisikiye, kuna jambo lanikaba Mbwene linitatiziye, hapa,kwingine ni haba Yuongoza msimachoye, kama huu sio msiba Niambiye hala, itawezekanaje? Yezekanaje nambiye, kipofu yuwaongoza Wanamfuata wenziye, nyumaye wamfuatiza Iweje mwe machoye, afuate mja weye jiza? Niambiye hala, itawezekanaje? Yuwenda kwenye ndiaye, muendo wa kupapasa Kawa ategemewaye, insi likuki wamfwasa, Kama hawapotezeye, na mawi yakawakusa Niambiye hala itawezekanaje? Wajenda kimwulizaye, ni kupi pa kukwendea? Fi kawapa majibuye, ‘lo! Sioni pa kwendea!” Mjua ndia hijuiye, ije wale wamlungea? Niambiye hala itawezekanaje? Hujaona luja aliye, akitoa hata mwengo Akiita jamaaye, wakatoke zao chengo “mwizi huyu mbueneye”, wakamfuatiya mgongo Nambiye hala, itawezekanaje? Mwizi kufata mwenziye, kuzifuata nyendoze Ameishika simeye, haja ni akamkomeze Wanyofu wafuatiye, na luja yuwaongoze, Nambiye hala, itawezekanaje? Boza kawa ajuaye, akayashika madaraka Mwamuzi kawa ni yeye, mwe’enzi na
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!