Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali Stendi unipe hidaya sipendi kutenda hili Sipendi mimi kucheka Sipendi mimi kucheka, kuchekea mawi Sipendi na ya dhihaka, kwangu nyemi hiwi Sipendi kwa hakika, mwovu kistawika Halafuye nikacheka! Masikini akiteswa Yatima akinyanyaswa Mnyonge naye akinyonywa Sipendi hata ikiwa Unazonguvu najuwa Na hili sitatekezwa Mbona lakini nicheke, kwayo furaha? Na wewe ukajiweke, uli na siha? Na yatima ali pweke, wa anahaha? Amenyimwa haki yake, hanayo raha! Na moyo wangu ucheke, kwa ha,ha,ha! Kucheka kwa kucheka Mimi katu sitacheka
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!