Vingine kama kuliwa,vinono na vitamu Vinywewa au tafunwa,vinavyokutia hamu A cha hata ungapawa, viwavyo navyo haramu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, uindhari binadamu, Vingine havitaliwa, visikuletee hukumu Ulapo vikaliliwa, vitakugeuka sumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, punguza yako hamumu, Visiwe vinyang’anywa, gharama yake ni ngumu Vingapo hata kufichwa, kamwe navyo havidumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, vingine kwa utalamu, Vikawa havitambuwa, ashaona Mungu Karimu, Hakika vitatapikwa, peupe mbe’ ya kaumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Wamalwa Kevin Mlokole Mulumbi FLTA alumni 2010/2011
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!