Skip to main content

Posts

Showing posts from June 12, 2011

Buriani swahiba

Siku pitile ayami, ukumbi sijasimama Sijajitokea mimi, hata kauli kusema Leo najiamba aimi, mbona sitasema lojema! Niutunge na ulimi, n’nene ya yangu mtima Kisema ni fika mimi, nimeipata naima Mola ameshanihami, menikumbuka Karama Kakomesha zangu kemi, kanondolea nakama Ameshanipa mimi, wangu alo pa mtima Ndio ukawa usemi, ninavyompenda Nelima Nilitasema kwa semi, waja waje kusoma Kuwa sina masghara mi’, nitampenda daima Bure bure siungami, sivyo singesema ‘metujalia we nami, katupa nyota njema Kajaazia na nyemi, na kila lililojema Huba likasibu kumi,nyoyo zikafungama Tupendane kwa ujumi, wala kwa nadama Sa’ wakati mewadiya, wangu mimi kuhama Nenda ughaibuniya, kwa mwaka huu mzima Sivyo nivyodhaniya, kuwa mapenzi huuma kawa tabu kwachaniya, japo   kweli ni lazima Nomba hili nijuliya, nakuenzi kwa gharama Hadi muhla wa kuuya, hubetu limesimama Limefurikia ghaya, zaidi ya takadama Kwa sasa buriani mbuya, ni mwiya wa kuchama Hili nakuahidiya, kukupenda kwa daima Nalo ninashikiliya