Skip to main content

Posts

Showing posts from February 26, 2012

penzi

penzi la kulazimisha,lina gharama, kando na kukalifisha, linakukama, na linakufilisisha, likakukwama, hadi likakubakisha, u litima aimi nakujulisha, uwe salama usipende kujishasha, na kwa lazima penda anorejesha, nayo kheshima huba ja hili hukosha, wako mtima ... mbwene hoa walopenda, kwa kusukuma, hatimaye zao zanda, wakaziuma, kumbe hao walopenda, wamewahama amwalio zimeenda, sa' wamezama