Toka Hegi yasikika, imelia parapanda Wafike walotajika, wasilimatie kwenda Majina waliandika, na ila walizotenda Waache kuhemeka, ili siku ya ulifi Nawaasa wahusika, waziache propaganda Hifai kulalamika, kila wanakokuenda Wengine tope kupaka, jukwaani wakipanda Wakuache kupayuka, ili siku ya ulifi Wenyewe waliyataka, mbegu mbaya walipanda Na chuki waliipika, ikaiva na kuvunda Na Umma ukagawika, maovu ukajitenda Sasa wana jakajaka, ili siku ya ulifi Mahuluki bila shaka, huvuna ‘lichopanda Na maji ukiyateka, uyanywe yote mafunda Na koo ikikabika, shauriyo ‘liyaenda Ela watawajibika, ili siku ya ulifi Wacheni kutikatika, kotekote mukiranda Mwakutaka kusifika, wafuasi mwawawinda Mwashinda kunung’unika, na mambo munayapinda Ishara ya kutishika, ili siku ya Ulifi Kama ni kutakasika, ni heri mkatuenenda Ghofira mkatutaka, tukawapa tukipenda Mumwombe Mahuluka, faraja akawatenda Badala ya kutimuka, ili siku ya ulifi Hitaaihirishika, siku ya ndege kupanda Mkayajibu mashtaka, ya zenu ila
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!