Skip to main content

Posts

Showing posts from November 14, 2010

yawezekanaje?

Nomba mkanisikiye, kuna jambo lanikaba Mbwene linitatiziye, hapa,kwingine ni haba Yuongoza msimachoye, kama huu sio msiba Niambiye hala, itawezekanaje? Yezekanaje nambiye, kipofu yuwaongoza Wanamfuata wenziye, nyumaye wamfuatiza Iweje mwe machoye, afuate mja weye jiza? Niambiye hala, itawezekanaje? Yuwenda kwenye ndiaye, muendo wa kupapasa Kawa ategemewaye, insi likuki wamfwasa, Kama hawapotezeye, na mawi yakawakusa Niambiye hala itawezekanaje? Wajenda kimwulizaye, ni kupi pa kukwendea? Fi kawapa majibuye, ‘lo! Sioni pa kwendea!” Mjua ndia hijuiye, ije wale wamlungea? Niambiye hala itawezekanaje? Hujaona luja aliye, akitoa hata mwengo Akiita jamaaye, wakatoke zao chengo “mwizi huyu mbueneye”, wakamfuatiya mgongo Nambiye hala, itawezekanaje? Mwizi kufata mwenziye, kuzifuata nyendoze Ameishika simeye, haja ni akamkomeze Wanyofu wafuatiye, na luja yuwaongoze, Nambiye hala, itawezekanaje? Boza kawa ajuaye, akayashika madaraka Mwamuzi kawa ni yeye, mwe’enzi na