‘Meandika nikujibu, ulouliza mwenzangu Kwelezeto nastahabu, welewe kauli yangu Kupenda nini sababu, umenisaili tangu Sikupendi kwa kupenda, ni kwa kuwa nakupenda Na maadamu hu bubu, utashiba jibu langu Kukupenda si ajabu, wan’saliti moyo wangu Mapenzi yaliusibu, kaubwaga wangu wangu Sikupendi kwa kupenda, ni kwa kuwa nakupenda Wala sinistaajabu, hikuwa kupenda kwangu Ngejua huba lan’karibu, ngelikaa ange kwa rungu Likija nilidhurubu, lisitwae mtima wangu Sikupendi kwa kupenda, ni kwa kuwa nakupenda Navyokupenda habubu, hujapendwa vile tangu Kwangu uli kama shabu, kunitakasa uchungu Kan’ridhie nawe hebu, ukubalie hayangu Sikupendi kwa kupenda, ni kwa kuwa nakupenda Hukuwazia ghalibu, fikra tele kwa mafungu Kitamani un’karibu, niwe wako uwe wangu Viate vyako ‘sababu, vilok’zinga ja magugu Sikupendi kwa kupenda, ni kwa kuwa nakupenda Hujui ngapi hesabu, n’mejipinda pali mvungu N’kililia lako jibu, litalon’toa kiwingu Uwele likanitibu, mato yao
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!