Niskize kote mlipo, niwape huno ujuzi Siku ya kura ijapo, ‘kiteuwa viongozi Kabila zetu zingapo, nyingi baidi ki’zazi Tutunze kenya iwepo, baada ya uchaguzi Na siasa tupigapo, tusitiye machokozi, kila mwahala twendapo, tudhihirishe wongozi, na wala sio matapo, ya kuzua machukizi, Hi' kenya itakuwapo, baada ya uchaguzi. Wazi mwajuwa malipo, ya kuzua uchafuzi, na kujifanya mapopo, tusiyatie maozi, ela yatendwe tulipo, wengi kawa wakimbizi, twataka kenya iwepo, baada ya uchaguzi kataa vidingapopo, vya kuzua uchochezi nao hawatakuwapo, tukichomana kwa mionzi wakipoa kwao pepo, nasi twazipiga kwenzi tuombe Kenya iwepo, baada ya uchaguzi Sisemi kupita hapo, menikaba usingizi, na chini nijilazapo, nawaasa wasikizi, kila mwahala mlipo, tusirudiye ya juzi, ili kenya ikawepo, baada ya uchaguzi. K.W Wamalwa Mlokole Mlumbi Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!