Nudhumu ninaiunda, ya mtimani kukuamba Yakufike ulikowanda, ujue yanonikumba Ninakwita uloenda, mbali ulikotamba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda Kufikiri nimeshinda, nazuzuika ja mshamba Sikwachi kukupenda, hata nizinge kwa ndumba Suhuba imenitanda, nisikiye nakuomba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda Fuadi imekuganda, hibanduki kama gamba Kama maua ya nyanda, imeshachanua tumba Ndo sikomi kukuwinda, na tungo nikilumba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda Mwendo naziuma zanda, kwa kukukosa mchumba Atiati yanipanda, nawazia kwenda kamba Nishaifikia kenda, kama kuhesabu namba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!