Skip to main content

Posts

Showing posts from 2011

vingawa vyaliwa

Vingine kama kuliwa,vinono na vitamu Vinywewa au tafunwa,vinavyokutia hamu A cha hata ungapawa, viwavyo navyo haramu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, uindhari binadamu, Vingine havitaliwa, visikuletee hukumu Ulapo vikaliliwa, vitakugeuka sumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, punguza yako hamumu, Visiwe vinyang’anywa, gharama yake ni ngumu Vingapo hata kufichwa, kamwe navyo havidumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, vingine kwa utalamu, Vikawa havitambuwa, ashaona Mungu Karimu, Hakika vitatapikwa, peupe mbe’ ya kaumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Wamalwa Kevin Mlokole Mulumbi FLTA alumni 2010/2011

Yana wenyewe

Makonde ya usuhuba, hayo yanao wenyewe Yanataka waloshiba, wakapandwa na viwewe Aimi wa nguvuhaba! sezi viwavu n'waniwe Huba ni la wa manguvu, n'lokifyefye najitowa N'lokifyefye najitowa, niachiye wenye nguvu Sitwai ningapawa, nachia yangu makovu Kumbe hayanayo dawa, yenye  kuleta utuvu Vikumbo vyayo mapenzi, vyahitaji wenye navyo Vyahitaji wenye navyo, wanotumia ja vyambo, Ukicheza nao ovyo, hutohimili makumbo Walai mja mimi sivyo, lau n'katowa matumbo Masumbwi ya huba n'yao, wenye mbinu za mikono Wenye mbinu za mikono, wajitenda pasi indha Wajuzi wa mavongono, hini kwao ndio ladha Kwazo kucha na vijino, wamewaatua kadha Mafundo yayo mahaba, ni ya wale wasimoyo Ni ya wale wasimoyo, walotasa wa hisia Ndio walo na   uchoyo, waja wanojitakia Huwezi ngapiga mbio, au kilema takutia Una kani chache flani, kana uwachie wao Kana uwachie wao, nakwamba ni wachokozi Kila kito ni cha kwao, sivyo wakulize chozi Nawajua watu zao, mbwene na yangu maozi

Buriani swahiba

Siku pitile ayami, ukumbi sijasimama Sijajitokea mimi, hata kauli kusema Leo najiamba aimi, mbona sitasema lojema! Niutunge na ulimi, n’nene ya yangu mtima Kisema ni fika mimi, nimeipata naima Mola ameshanihami, menikumbuka Karama Kakomesha zangu kemi, kanondolea nakama Ameshanipa mimi, wangu alo pa mtima Ndio ukawa usemi, ninavyompenda Nelima Nilitasema kwa semi, waja waje kusoma Kuwa sina masghara mi’, nitampenda daima Bure bure siungami, sivyo singesema ‘metujalia we nami, katupa nyota njema Kajaazia na nyemi, na kila lililojema Huba likasibu kumi,nyoyo zikafungama Tupendane kwa ujumi, wala kwa nadama Sa’ wakati mewadiya, wangu mimi kuhama Nenda ughaibuniya, kwa mwaka huu mzima Sivyo nivyodhaniya, kuwa mapenzi huuma kawa tabu kwachaniya, japo   kweli ni lazima Nomba hili nijuliya, nakuenzi kwa gharama Hadi muhla wa kuuya, hubetu limesimama Limefurikia ghaya, zaidi ya takadama Kwa sasa buriani mbuya, ni mwiya wa kuchama Hili nakuahidiya, kukupenda kwa daima Nalo ninashikiliya

Bin-Adamu

Mimi Natakadamu ino nudhumu Nikayaambe yalomuhimu Yanotaja ghilba za bin-Adamu Wa kuhalalisha yalokharamu kufaidi yake tamaa na hamumu Yalo mema kayatiya sumu Na kuwaseta walomaamumu Wakijigeuza sanamu Wakisahau wali wanadamu Kataka ibada kwa kaumu Wadhani Takwepa luhdi wakisha humu Watakinza ya Mungu Kalamu Kwamba Muhuluku hafahamu ati hiyeyuki fuadi ngumu Ila Wendelepi siku ya hukumu? Watapokwima mbele ya Hakimu Kulipiya wao udhalimu Kama si nyoto za Jehanamu? Zitakao waunguza kwa zamu Zikisha lamba mifupa na damu Watauma zanda na kujilaumu kwa wao utimamu wa wazimu ©Wamalwa
Naja kwa jina lake Mungu Kwamba yalo moyoni mwangu Yaliyo tamu na machungu Uje kulimuka mwenzangu Ukituliana nikwambie Nitasema pasi kificha Nikuonye bila kukucha Kuwa jambo ‘kikufikicha La ukweli uliochacha Nihisani uniambie Hakuna aliyenyooka Muenda asiyeteguka Kwa wazo au kutamuka Miye pia wakupunguka Ukiona ila nambie Ni wa chira asoonyeka Muambae asokanyika Mara tatu hajaambika Atajuta akikutika Zamu yako ni umwambie Ukweli mchungu huuma Na hugharimu kuusema Ela ni dawa ya hatima Huja kuuponya mtima Ukiwa nao   we’nambie Kanyo lako ukichelea Ukiniona nakosea Kwa Mungu ukijitetea Hesabu utanitolea Kujitoa ila,nambie Niambie liwapo chungu Usinifumbie mizungu Walau likawe uchengu Mwanga wa maozi yangu Usiche kuindha nambie Natua hapa nikuindha Kwa hayo maonyo kadha Kuyashika kwako faradha Maishani yakupe ladha Ela hikufai, nambie © Wamalwa

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

Nikome Uniambae

Kama utanisikiya, nambe haya kukuindha Majambo nilowaziya, si moja ila ni kadha Yenye heri kufaidiya, ungayafwata faradha Kama sivyo swahibiya, nikome nambae Kama uli wa kukimbiya, na haraka za vitendo, Naona huton’faiya, zangu ni   za pole nyendo Mambo mi’ hiyapaniya, haraka ina uvundo Kama hutosubiriya, nikome uniambae Kama limi umenoya, linakata kama msu Na Inda   kutapakaya, ndugu kuwagawa nusu Nyoyo kuwakereya, na kukeeza ja kisu Kama ndugu kuchukiya, nikome uniambae Kama huli wakupenda, umejaa inda na inadi Chuki imejenga banda, imekingama f uadi Sin’tiye kwayo mawanda, naona umeshadidi Kama hutogeukiya, nikome uniambae

He fears Nothing!

He told me he fears nothing Looking at me without blinking And gave me so long a list Of things he fears not From the deep blackness of the night To the horrific steep of the deep He fears not the most terrible beast of the land For once he tore the lion by his bare hands He fears nothing Not to mention the leviathan he has seen not But, I fear ‘nothing’ more than anything More than what he has in his inventory Because nothing is something to fear When I think of its loud silence Loud enough to wake the dead The emptiness of nothing! The darkness of nothing! Oh, I fear nothing, than anything Oh that I will never meet it And be swallowed in its hollowness Where nothing really is Where the present and future meets And devour each other to nothingness You should fear ‘Nothing’   For in her embrace the sun halts its light And the budded roses blossom not And the beauty of the setting sun becomes gross When u don’t have ground beneath To old your feeble knees Neither heaven above overlook

‘Twas time to die

Twas not time to die When I thought I would After falling in the snare of the sly And my affection such robbed When she played with my heart Twas not time to die When I sunk in despair When my world had crumbled And gone was the essence of life Could I cry enough of a tear? Could I brood enough in gloom? When the most tender The most delicate of my person Has been put on play!! My silence was so loud My wail was so silent I only, only I could understand The wordless speech of my heart And my ears could hear the message And the wisdom of the innermost That at the end of this all Is where the beginning lay Thus, I learnt to laugh in my tears I learnt to live in my dying. Is it not with death that we tell what life is Is it not with weakness that we define strength? Or with betrayal that we appreciate trust? And with hate that love stands out I learnt to wait, just a little longer Then my love will bloom again Twas time to learn life Twas not time to die yet!

Wangu ulojisunda

Nudhumu ninaiunda, ya mtimani kukuamba Yakufike ulikowanda, ujue yanonikumba Ninakwita uloenda, mbali ulikotamba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda Kufikiri nimeshinda, nazuzuika ja mshamba Sikwachi kukupenda, hata nizinge kwa ndumba Suhuba imenitanda, nisikiye nakuomba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda Fuadi imekuganda, hibanduki kama gamba Kama maua ya nyanda, imeshachanua tumba Ndo sikomi kukuwinda, na tungo nikilumba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda Mwendo naziuma zanda, kwa kukukosa mchumba Atiati yanipanda, nawazia kwenda kamba Nishaifikia kenda, kama kuhesabu namba Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda

karama

Siendi Kinyumenyume Siendi kinyumenyume kama mshamba wa kimeme Ndoto yanitia shime Japo nagwa nisimame Nikatwete na niheme N'takakania kiume Nikaziangushe ngome Na, Nitasongesha milima Ndiani ilosimama Nitashinda wanonizima Wanonifisha na mtima Nitafika hata kama Nuru zote zimezima Nacho kiza kusakama Nitaifikia yangu karama

Uniambae!

Kama utanisikiya, nambe haya kukuindha Majambo nilowaziya, si moja ila ni kadha Yenye heri kufaidiya, ungayafwata faradha Kama sivyo swahibiya, kanikome unambae Kama uli wa kukimbiya, na haraka za vitendo, Naona huton’faiya, zangu ni za pole nyendo Mambo mi’ hiyapaniya, haraka ina uvundo Kama hutosubiriya, unikome uniambae Kama limi umenoya, linakata kama msu Na Inda kutapakaya, ndugu kuwagawa nusu Nyoyo kuwakereya, na kukeeza ja kisu Kama ndugu kuchukiya, unikome uniambae

Siku ya Ulifi

Toka Hegi yasikika, imelia parapanda Wafike walotajika, wasilimatie kwenda Majina waliandika, na ila walizotenda Waache kuhemeka, ili siku ya ulifi Nawaasa wahusika, waziache propaganda Hifai kulalamika, kila wanakokuenda Wengine tope kupaka, jukwaani wakipanda Wakuache kupayuka, ili siku ya ulifi Wenyewe waliyataka, mbegu mbaya walipanda Na chuki waliipika, ikaiva na kuvunda Na Umma ukagawika, maovu ukajitenda Sasa wana jakajaka, ili siku ya ulifi Mahuluki bila shaka, huvuna ‘lichopanda Na maji ukiyateka, uyanywe yote mafunda Na koo ikikabika, shauriyo ‘liyaenda Ela watawajibika, ili siku ya ulifi Wacheni kutikatika, kotekote mukiranda Mwakutaka kusifika, wafuasi mwawawinda Mwashinda kunung’unika, na mambo munayapinda Ishara ya kutishika, ili siku ya Ulifi Kama ni kutakasika, ni heri mkatuenenda Ghofira mkatutaka, tukawapa tukipenda Mumwombe Mahuluka, faraja akawatenda Badala ya kutimuka, ili siku ya ulifi Hitaaihirishika, siku ya ndege kupanda Mkayajibu mashtaka, ya zenu ila