Naililia kenya, nchi yangu laazizi fuadi yan'tekenya, kuzuwiya siwezi na ajizi sitofanya, kumwomba mwenyezi aiauni kenya, toka kwa wafinyanzi so wema nakukanya, hawano wafinyanzi kwa hila waibinya, na kutiya makunyanzi sao waibambanya, kukuza yao enzi si wema wanasinya, twawajua ni wafyonzi Niya zao si chanya, n'za kuzua machozi wajuzi wajifanya, hawanao ujuzi amwali wakusanya, wazizoa za wizi wala wakitapanya, nasi twala majonzi
Ukumbi huu unalenga kukupa uhondo wa sanaa ya ushairiwa kiswahili. utapata mashairi mengi ambayo nimeyatunga mwenye na mengine yakachapisha kwenye Taifa Leo. Kando na haya utapata kufaidika na makala ya kukuhimiza ikiwa wewe ni mkrsito. Yamkini nitalenga kuwakidhia mahitaji mbalimbali ya kukujengeni. ****** Get entertained with lots of Swahili poems posted daily. Watch movies by going to "movies!!! button. Lots of Items to buy instantly at "Nunua/Buy Items" page and Lots of other good deals!