Skip to main content

Posts

Showing posts from October 17, 2010

Naililia

Naililia kenya, nchi yangu laazizi fuadi yan'tekenya, kuzuwiya siwezi na ajizi sitofanya, kumwomba mwenyezi aiauni kenya, toka kwa wafinyanzi so wema nakukanya, hawano wafinyanzi kwa hila waibinya, na kutiya makunyanzi sao waibambanya, kukuza yao enzi si wema wanasinya, twawajua ni wafyonzi Niya zao si chanya, n'za kuzua machozi wajuzi wajifanya, hawanao ujuzi amwali wakusanya, wazizoa za wizi wala wakitapanya, nasi twala majonzi