Naililia kenya, nchi yangu laazizi
fuadi yan'tekenya, kuzuwiya siwezi
na ajizi sitofanya, kumwomba mwenyezi
aiauni kenya, toka kwa wafinyanzi
so wema nakukanya, hawano wafinyanzi
kwa hila waibinya, na kutiya makunyanzi
sao waibambanya, kukuza yao enzi
si wema wanasinya, twawajua ni wafyonzi
Niya zao si chanya, n'za kuzua machozi
wajuzi wajifanya, hawanao ujuzi
amwali wakusanya, wazizoa za wizi
wala wakitapanya, nasi twala majonzi
fuadi yan'tekenya, kuzuwiya siwezi
na ajizi sitofanya, kumwomba mwenyezi
aiauni kenya, toka kwa wafinyanzi
so wema nakukanya, hawano wafinyanzi
kwa hila waibinya, na kutiya makunyanzi
sao waibambanya, kukuza yao enzi
si wema wanasinya, twawajua ni wafyonzi
Niya zao si chanya, n'za kuzua machozi
wajuzi wajifanya, hawanao ujuzi
amwali wakusanya, wazizoa za wizi
wala wakitapanya, nasi twala majonzi
Comments