Nomba mkanisikiye, kuna jambo lanikaba
Mbwene linitatiziye, hapa,kwingine ni haba
Yuongoza msimachoye, kama huu sio msiba
Niambiye hala, itawezekanaje?
Yezekanaje nambiye, kipofu yuwaongoza
Wanamfuata wenziye, nyumaye wamfuatiza
Iweje mwe machoye, afuate mja weye jiza?
Niambiye hala, itawezekanaje?
Yuwenda kwenye ndiaye, muendo wa kupapasa
Kawa ategemewaye, insi likuki wamfwasa,
Kama hawapotezeye, na mawi yakawakusa
Niambiye hala itawezekanaje?
Wajenda kimwulizaye, ni kupi pa kukwendea?
Fi kawapa majibuye, ‘lo! Sioni pa kwendea!”
Mjua ndia hijuiye, ije wale wamlungea?
Niambiye hala itawezekanaje?
Hujaona luja aliye, akitoa hata mwengo
Akiita jamaaye, wakatoke zao chengo
“mwizi huyu mbueneye”, wakamfuatiya mgongo
Nambiye hala, itawezekanaje?
Mwizi kufata mwenziye, kuzifuata nyendoze
Ameishika simeye, haja ni akamkomeze
Wanyofu wafuatiye, na luja yuwaongoze,
Nambiye hala, itawezekanaje?
Boza kawa ajuaye, akayashika madaraka
Mwamuzi kawa ni yeye, mwe’enzi na mamulaka
I’je asejua naye, maarifa kuyaweka
Nambiye hala, itawezekanaje?
Mbona asejua naye, asijue asolijua
Ataijua haliye, akawa wakuamua?
Japo yuwadai yeye, utumwa kajifungua
Nambiye hala, itawezekanaje?
Sasa sema nijibiye, nyama mekufungiya
Pali na asejuaye, hajui hajifahamiya
Naye insi ajuaye, hajui achojijuiya!
Nambiye hala, itawezekanaje?
Mbwene linitatiziye, hapa,kwingine ni haba
Yuongoza msimachoye, kama huu sio msiba
Niambiye hala, itawezekanaje?
Yezekanaje nambiye, kipofu yuwaongoza
Wanamfuata wenziye, nyumaye wamfuatiza
Iweje mwe machoye, afuate mja weye jiza?
Niambiye hala, itawezekanaje?
Yuwenda kwenye ndiaye, muendo wa kupapasa
Kawa ategemewaye, insi likuki wamfwasa,
Kama hawapotezeye, na mawi yakawakusa
Niambiye hala itawezekanaje?
Wajenda kimwulizaye, ni kupi pa kukwendea?
Fi kawapa majibuye, ‘lo! Sioni pa kwendea!”
Mjua ndia hijuiye, ije wale wamlungea?
Niambiye hala itawezekanaje?
Hujaona luja aliye, akitoa hata mwengo
Akiita jamaaye, wakatoke zao chengo
“mwizi huyu mbueneye”, wakamfuatiya mgongo
Nambiye hala, itawezekanaje?
Mwizi kufata mwenziye, kuzifuata nyendoze
Ameishika simeye, haja ni akamkomeze
Wanyofu wafuatiye, na luja yuwaongoze,
Nambiye hala, itawezekanaje?
Boza kawa ajuaye, akayashika madaraka
Mwamuzi kawa ni yeye, mwe’enzi na mamulaka
I’je asejua naye, maarifa kuyaweka
Nambiye hala, itawezekanaje?
Mbona asejua naye, asijue asolijua
Ataijua haliye, akawa wakuamua?
Japo yuwadai yeye, utumwa kajifungua
Nambiye hala, itawezekanaje?
Sasa sema nijibiye, nyama mekufungiya
Pali na asejuaye, hajui hajifahamiya
Naye insi ajuaye, hajui achojijuiya!
Nambiye hala, itawezekanaje?
Comments