Skip to main content

Popular posts from this blog

yawezekanaje?

Nomba mkanisikiye, kuna jambo lanikaba Mbwene linitatiziye, hapa,kwingine ni haba Yuongoza msimachoye, kama huu sio msiba Niambiye hala, itawezekanaje? Yezekanaje nambiye, kipofu yuwaongoza Wanamfuata wenziye, nyumaye wamfuatiza Iweje mwe machoye, afuate mja weye jiza? Niambiye hala, itawezekanaje? Yuwenda kwenye ndiaye, muendo wa kupapasa Kawa ategemewaye, insi likuki wamfwasa, Kama hawapotezeye, na mawi yakawakusa Niambiye hala itawezekanaje? Wajenda kimwulizaye, ni kupi pa kukwendea? Fi kawapa majibuye, ‘lo! Sioni pa kwendea!” Mjua ndia hijuiye, ije wale wamlungea? Niambiye hala itawezekanaje? Hujaona luja aliye, akitoa hata mwengo Akiita jamaaye, wakatoke zao chengo “mwizi huyu mbueneye”, wakamfuatiya mgongo Nambiye hala, itawezekanaje? Mwizi kufata mwenziye, kuzifuata nyendoze Ameishika simeye, haja ni akamkomeze Wanyofu wafuatiye, na luja yuwaongoze, Nambiye hala, itawezekanaje? Boza kawa ajuaye, akayashika madaraka Mwamuzi kawa ni yeye, mwe’enzi na...
Hajafua Dafu Kama alivyo msasi, endaye kuwinda huwa Jenda kwa hamu na kasi,  kilenga kunasa njiwa Zimpatapo khasaisi, kumbe ndege hakutuwa Bado dafu hajafuwa, Mdavadi kijita Mesi Kwa makeke kahujuru, kuitafuta muruwa, Aionje hewa huru, kumbe nako  haikuwa Akapunjwa na Uhuru, alotaka kahiniwa Kabaki mechachamuwa,   zimwishiye furufuru Lisadiki sakumbimbi, walomlisha vongono  Kapotoshwa na wachimbi, na waja wasimaono Kamtowa kwenye kambi, alikopata usono Sasa yuasaga meno, akiulizwa haambi Kendea virambaramba, vichicha vya ukoloni Ndio navyo yuagamba, kuwa farasi mbioni Ni kama guo la mtumba, ‘pambwe mwari arusini Hata hawiki mjini, KANU jogoo wa shamba Nakoma wasiniambe, wanitusi wajuao Nachelea wanichimbe, wan’dhuru vibarakao Ila n’metowa ujumbe, wamwindhe nahodha wao “Sijetuwa meli yao, kwenye kaburi chimbe K.W Wamalwa Mlokole Mlumbi Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison

Waziri

Nina hili la kujua, mkaniwekee dhahiri, Utata mkautatua, mkanipeni na fasiri Ni jambo la nisumbua, lanikiera kifikiri Anacho nini waziri, au waziri ni wa-siri? Ni nini amekificha, kama waziri ni wa-siri? Nini anachokicha, asijiweke dhahiri? Wazimu umemchacha, kawa wakutofikiri? Augua nini waziri, au ana bawasiri? Mbona hana razini, ‘wapo hana bawasiri? Mbona yeye hatuoni, madhila yamekithiri! Anatutiya shimoni, mwa madhila na shari Waziri kweli waziri, au yeye wa-aziri? Amepania hakomi, kusitisha athari, Zimezidi mara kumi, athari za ubepari, Anajinaki ni msomi, kwetu siye ajibari Kujua mie nashindwa, ni waziri au hasiri? Ni nani wahasiriwa, awapo yeye hasiri? Wewe usiye jaliwa, mja usiye na kheri Mimi nisiyejengewa, Kama hilo lake kasri Ni wewe na mimi yakhe, tunaopata athari Basi kazi yake nini, anayotenda waziri? Au kutamba garini, akienda nyigi ziari Kwenda mahotelini, na kulewa chakari, Nijibu anani waziri, achofanya barazani