Skip to main content

Wangu ulojisunda

Nudhumu ninaiunda, ya mtimani kukuamba
Yakufike ulikowanda, ujue yanonikumba
Ninakwita uloenda, mbali ulikotamba
Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda

Kufikiri nimeshinda, nazuzuika ja mshamba
Sikwachi kukupenda, hata nizinge kwa ndumba
Suhuba imenitanda, nisikiye nakuomba
Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda

Fuadi imekuganda, hibanduki kama gamba
Kama maua ya nyanda, imeshachanua tumba
Ndo sikomi kukuwinda, na tungo nikilumba
Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda

Mwendo naziuma zanda, kwa kukukosa mchumba
Atiati yanipanda, nawazia kwenda kamba
Nishaifikia kenda, kama kuhesabu namba
Jifaraghua e nyonda, wangu uliyejisunda

Comments

Popular posts from this blog

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Yupi mwenye haki

1.           Yupi ale mahuluki, asiye kuwa na doa Ni yupi ale na haki, asiye wa kukosoa Mja ambaye hakiuki, akawa wa kupotea Hayupo muenye haki, maki wote meondoa 2.           Yupi asiye wa kosa, mnyofu wazo nyendo, Awapo aseme sasa, akajinegee kando, Yule ale jitakasa, safi hanao uvundo Hakuna asiyekosa, kwa kauli na matendo 3.           Sijaona aliyejitosha, akahimili nafsiye Insi asejikunguisha, ulimi kwa kauliye Nani asiye keresha, kubughudhi muumbaye Ila tu akajikosha, akatubia dhambiye 4.           Nani asiyekunguwaa, kwa fikra ya moyoni Kunaye asiye na waa, lilofichama wazoni? Awe mja anayefaa, kwa Rabana machoni? Wote wamepunguwaa, utukufu hawaoni.   5.           Yupi basi wa kupona? amchaye Mola wake Nani ataka...