Vingine kama kuliwa,vinono na vitamu
Vinywewa au tafunwa,vinavyokutia hamu
A cha hata ungapawa, viwavyo navyo haramu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Vingine kama vyaliwa, uindhari binadamu,
Vingine havitaliwa, visikuletee hukumu
Ulapo vikaliliwa, vitakugeuka sumu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Vingine kama vyaliwa, punguza yako hamumu,
Visiwe vinyang’anywa, gharama yake ni ngumu
Vingapo hata kufichwa, kamwe navyo havidumu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Vingine kama vyaliwa, vingine kwa utalamu,
Vikawa havitambuwa, ashaona Mungu Karimu,
Hakika vitatapikwa, peupe mbe’ ya kaumu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Wamalwa Kevin
Mlokole Mulumbi
FLTA alumni 2010/2011
Vinywewa au tafunwa,vinavyokutia hamu
A cha hata ungapawa, viwavyo navyo haramu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Vingine kama vyaliwa, uindhari binadamu,
Vingine havitaliwa, visikuletee hukumu
Ulapo vikaliliwa, vitakugeuka sumu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Vingine kama vyaliwa, punguza yako hamumu,
Visiwe vinyang’anywa, gharama yake ni ngumu
Vingapo hata kufichwa, kamwe navyo havidumu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Vingine kama vyaliwa, vingine kwa utalamu,
Vikawa havitambuwa, ashaona Mungu Karimu,
Hakika vitatapikwa, peupe mbe’ ya kaumu
Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu
Wamalwa Kevin
Mlokole Mulumbi
FLTA alumni 2010/2011
Comments