Skip to main content

Kenya Itakuwepo

Niskize kote mlipo, niwape huno ujuzi
Siku ya kura ijapo, ‘kiteuwa viongozi
Kabila zetu zingapo, nyingi baidi ki’zazi
Tutunze kenya iwepo, baada ya uchaguzi

Na siasa tupigapo, tusitiye machokozi,
kila mwahala twendapo, tudhihirishe wongozi,
na wala sio matapo, ya kuzua machukizi,
Hi' kenya itakuwapo, baada ya uchaguzi.

Wazi mwajuwa malipo, ya kuzua uchafuzi,
na kujifanya mapopo, tusiyatie maozi,
ela yatendwe tulipo, wengi kawa wakimbizi,
twataka kenya iwepo, baada ya uchaguzi

kataa vidingapopo, vya kuzua uchochezi
nao hawatakuwapo, tukichomana kwa mionzi
wakipoa kwao pepo, nasi twazipiga kwenzi
tuombe Kenya iwepo, baada ya uchaguzi

Sisemi kupita hapo, menikaba usingizi,
na chini nijilazapo, nawaasa wasikizi,
kila mwahala mlipo, tusirudiye ya juzi,
ili kenya ikawepo, baada ya uchaguzi.

K.W Wamalwa
Mlokole Mlumbi
Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison

Comments

Popular posts from this blog

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

mtu hafi kupenda

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

penzi

penzi la kulazimisha,lina gharama, kando na kukalifisha, linakukama, na linakufilisisha, likakukwama, hadi likakubakisha, u litima aimi nakujulisha, uwe salama usipende kujishasha, na kwa lazima penda anorejesha, nayo kheshima huba ja hili hukosha, wako mtima ... mbwene hoa walopenda, kwa kusukuma, hatimaye zao zanda, wakaziuma, kumbe hao walopenda, wamewahama amwalio zimeenda, sa' wamezama