Niskize kote mlipo, niwape huno ujuzi
Siku ya kura ijapo, ‘kiteuwa viongozi
Kabila zetu zingapo, nyingi baidi ki’zazi
Tutunze kenya iwepo, baada ya uchaguzi
Na siasa tupigapo, tusitiye machokozi,
kila mwahala twendapo, tudhihirishe wongozi,
na wala sio matapo, ya kuzua machukizi,
Hi' kenya itakuwapo, baada ya uchaguzi.
Wazi mwajuwa malipo, ya kuzua uchafuzi,
na kujifanya mapopo, tusiyatie maozi,
ela yatendwe tulipo, wengi kawa wakimbizi,
twataka kenya iwepo, baada ya uchaguzi
kataa vidingapopo, vya kuzua uchochezi
nao hawatakuwapo, tukichomana kwa mionzi
wakipoa kwao pepo, nasi twazipiga kwenzi
tuombe Kenya iwepo, baada ya uchaguzi
Sisemi kupita hapo, menikaba usingizi,
na chini nijilazapo, nawaasa wasikizi,
kila mwahala mlipo, tusirudiye ya juzi,
ili kenya ikawepo, baada ya uchaguzi.
K.W Wamalwa
Mlokole Mlumbi
Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison
Siku ya kura ijapo, ‘kiteuwa viongozi
Kabila zetu zingapo, nyingi baidi ki’zazi
Tutunze kenya iwepo, baada ya uchaguzi
Na siasa tupigapo, tusitiye machokozi,
kila mwahala twendapo, tudhihirishe wongozi,
na wala sio matapo, ya kuzua machukizi,
Hi' kenya itakuwapo, baada ya uchaguzi.
Wazi mwajuwa malipo, ya kuzua uchafuzi,
na kujifanya mapopo, tusiyatie maozi,
ela yatendwe tulipo, wengi kawa wakimbizi,
twataka kenya iwepo, baada ya uchaguzi
kataa vidingapopo, vya kuzua uchochezi
nao hawatakuwapo, tukichomana kwa mionzi
wakipoa kwao pepo, nasi twazipiga kwenzi
tuombe Kenya iwepo, baada ya uchaguzi
Sisemi kupita hapo, menikaba usingizi,
na chini nijilazapo, nawaasa wasikizi,
kila mwahala mlipo, tusirudiye ya juzi,
ili kenya ikawepo, baada ya uchaguzi.
K.W Wamalwa
Mlokole Mlumbi
Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison
Comments