Naja kwa jina lake Mungu
Kwamba yalo moyoni mwangu
Yaliyo tamu na machungu
Uje kulimuka mwenzangu
Ukituliana nikwambie
Nitasema pasi kificha
Nikuonye bila kukucha
Kuwa jambo ‘kikufikicha
La ukweli uliochacha
Nihisani uniambie
Hakuna aliyenyooka
Muenda asiyeteguka
Kwa wazo au kutamuka
Miye pia wakupunguka
Ukiona ila nambie
Ni wa chira asoonyeka
Muambae asokanyika
Mara tatu hajaambika
Atajuta akikutika
Zamu yako ni umwambie
kweli mchungu huuma
Na hugharimu kuusema
Ela ni dawa ya hatima
Huja kuuponya mtima
Ukiwa nao we’nambie
Kanyo lako ukichelea
Ukiniona nakosea
Kwa Mungu ukijitetea
Hesabu utanitolea
Kujitoa ila,nambie
Niambie liwapo chungu
Usinifumbie mizungu
Walau likawe uchengu
Mwanga wa maozi yangu
Usiche kuindha nambie
Kwamba yalo moyoni mwangu
Yaliyo tamu na machungu
Uje kulimuka mwenzangu
Ukituliana nikwambie
Nitasema pasi kificha
Nikuonye bila kukucha
Kuwa jambo ‘kikufikicha
La ukweli uliochacha
Nihisani uniambie
Hakuna aliyenyooka
Muenda asiyeteguka
Kwa wazo au kutamuka
Miye pia wakupunguka
Ukiona ila nambie
Ni wa chira asoonyeka
Muambae asokanyika
Mara tatu hajaambika
Atajuta akikutika
Zamu yako ni umwambie
kweli mchungu huuma
Na hugharimu kuusema
Ela ni dawa ya hatima
Huja kuuponya mtima
Ukiwa nao we’nambie
Kanyo lako ukichelea
Ukiniona nakosea
Kwa Mungu ukijitetea
Hesabu utanitolea
Kujitoa ila,nambie
Niambie liwapo chungu
Usinifumbie mizungu
Walau likawe uchengu
Mwanga wa maozi yangu
Usiche kuindha nambie
Comments