Skip to main content

Niambie

Naja kwa jina lake Mungu
Kwamba yalo moyoni mwangu
Yaliyo tamu na machungu
Uje kulimuka mwenzangu
Ukituliana nikwambie

Nitasema pasi kificha
Nikuonye bila kukucha
Kuwa jambo ‘kikufikicha
La ukweli uliochacha
Nihisani uniambie

Hakuna aliyenyooka
Muenda asiyeteguka
Kwa wazo au kutamuka
Miye pia wakupunguka
Ukiona ila nambie

Ni wa chira asoonyeka
Muambae asokanyika
Mara tatu hajaambika
Atajuta akikutika
Zamu yako ni umwambie

kweli mchungu huuma
Na hugharimu kuusema
Ela ni dawa ya hatima
Huja kuuponya mtima
Ukiwa nao we’nambie

Kanyo lako ukichelea
Ukiniona nakosea
Kwa Mungu ukijitetea
Hesabu utanitolea
Kujitoa ila,nambie

Niambie liwapo chungu
Usinifumbie mizungu
Walau likawe uchengu
Mwanga wa maozi yangu
Usiche kuindha nambie

Comments

Popular posts from this blog

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

mtu hafi kupenda

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

penzi

penzi la kulazimisha,lina gharama, kando na kukalifisha, linakukama, na linakufilisisha, likakukwama, hadi likakubakisha, u litima aimi nakujulisha, uwe salama usipende kujishasha, na kwa lazima penda anorejesha, nayo kheshima huba ja hili hukosha, wako mtima ... mbwene hoa walopenda, kwa kusukuma, hatimaye zao zanda, wakaziuma, kumbe hao walopenda, wamewahama amwalio zimeenda, sa' wamezama