Shukrani!
Shukrani zangu jazila, kwa chama cha
NCOLTCL (nikotiko)
Akawajazi jaala, kwa kutupa mualiko
Tumeteremea kulla, tulosoma toka kwako
Sasa
tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
Sikomi
kuwahongera, walimu walofundisha
walivyojifunga
nira, ya maarifa kutupasha
Tuzijenge
mbinu bora, Kiswahili kufundisha
Sasa
tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
Mambo
hayo ni muhimu, mlotupasha uchao
Mliyeshusha
magumu, ya nadharia zao
Tuboreke
walimu, kwa wale tufudnishao
Sasa
tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
Hongera
mwalimu Kiarie, kwa kuonyesha mifano
Lisanza
nikusifie, kwazo sifa nono nono
Alwiya
zikufikie, ulivyokuwa mfano
Sasa
tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
Sikusahau
Atonia, kwa wako ukakamavu,
Jinsi
ulokakania, pasi kuonya ochovu
Uneemee
dunia, kwa kutupa wangavu
Sasa
tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
Wanafunzi
mlofika, shukrani nyingi sana
Kwenu kuwa
washirika, na mwiya wenu kupana
Na sisi
tukazoeka, na vipindi vilofana
Sasa
tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
Hongera Kesi, Kartika, na Melisa kwayo ari
Chelisi ulisikika, kwa ari na machachari
Nelisoni
naye Jaka (jack), pongezi kwa uhodari
Sasa
mmelishamuka, na mbinu kujifundisha
Nafasi
hiniruhusu, nikawataje kwa jina
Ingehalali kwa busu, ningewapa tangu jana
Silasi upate nusu, kisha
nimpe Diana
Kwani tumeshalimuka, na mbinu kujifundisha
Kwaheri ya kuonana, kirejea viamboni
Awatunze Maulana, tutaonana usoni
Na ari tumepashana, tuzidi kuikokeni
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha
©Mlokole Mlumbi
Kevin
Wamalwa
Chuo
Kikuu cha Wisconsin-Madison
Comments