Skip to main content

Kukrani!



Shukrani!
Shukrani zangu jazila, kwa chama cha NCOLTCL (nikotiko)
Akawajazi jaala, kwa kutupa mualiko
Tumeteremea kulla, tulosoma toka kwako
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

Sikomi kuwahongera, walimu walofundisha
walivyojifunga nira, ya maarifa kutupasha
Tuzijenge mbinu bora, Kiswahili kufundisha
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

Mambo hayo ni muhimu, mlotupasha uchao
Mliyeshusha magumu, ya nadharia zao
Tuboreke walimu, kwa wale tufudnishao
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

Hongera mwalimu Kiarie, kwa kuonyesha mifano
Lisanza nikusifie, kwazo sifa nono nono
Alwiya zikufikie, ulivyokuwa mfano
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

Sikusahau Atonia, kwa wako ukakamavu,
Jinsi ulokakania, pasi kuonya ochovu
Uneemee dunia, kwa kutupa wangavu
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

Wanafunzi mlofika, shukrani nyingi sana
Kwenu kuwa washirika, na mwiya wenu kupana
Na sisi tukazoeka, na vipindi vilofana
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

Hongera Kesi, Kartika, na Melisa kwayo ari
Chelisi ulisikika, kwa ari na machachari
Nelisoni naye Jaka (jack), pongezi kwa uhodari
Sasa mmelishamuka, na mbinu kujifundisha

Nafasi hiniruhusu, nikawataje kwa jina
Ingehalali kwa busu, ningewapa tangu jana
Silasi upate nusu, kisha nimpe Diana
Kwani tumeshalimuka, na mbinu kujifundisha

Kwaheri ya kuonana, kirejea viamboni
Awatunze Maulana, tutaonana usoni
Na ari tumepashana, tuzidi kuikokeni
Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha

©Mlokole Mlumbi
Kevin Wamalwa
Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison

Comments

Popular posts from this blog

Bin-Adamu

Mimi Natakadamu ino nudhumu Nikayaambe yalomuhimu Yanotaja ghilba za bin-Adamu Wa kuhalalisha yalokharamu kufaidi yake tamaa na hamumu Yalo mema kayatiya sumu Na kuwaseta walomaamumu Wakijigeuza sanamu Wakisahau wali wanadamu Kataka ibada kwa kaumu Wadhani Takwepa luhdi wakisha humu Watakinza ya Mungu Kalamu Kwamba Muhuluku hafahamu ati hiyeyuki fuadi ngumu Ila Wendelepi siku ya hukumu? Watapokwima mbele ya Hakimu Kulipiya wao udhalimu Kama si nyoto za Jehanamu? Zitakao waunguza kwa zamu Zikisha lamba mifupa na damu Watauma zanda na kujilaumu kwa wao utimamu wa wazimu ©Wamalwa

Siku ya Ulifi

Toka Hegi yasikika, imelia parapanda Wafike walotajika, wasilimatie kwenda Majina waliandika, na ila walizotenda Waache kuhemeka, ili siku ya ulifi Nawaasa wahusika, waziache propaganda Hifai kulalamika, kila wanakokuenda Wengine tope kupaka, jukwaani wakipanda Wakuache kupayuka, ili siku ya ulifi Wenyewe waliyataka, mbegu mbaya walipanda Na chuki waliipika, ikaiva na kuvunda Na Umma ukagawika, maovu ukajitenda Sasa wana jakajaka, ili siku ya ulifi Mahuluki bila shaka, huvuna ‘lichopanda Na maji ukiyateka, uyanywe yote mafunda Na koo ikikabika, shauriyo ‘liyaenda Ela watawajibika, ili siku ya ulifi Wacheni kutikatika, kotekote mukiranda Mwakutaka kusifika, wafuasi mwawawinda Mwashinda kunung’unika, na mambo munayapinda Ishara ya kutishika, ili siku ya Ulifi Kama ni kutakasika, ni heri mkatuenenda Ghofira mkatutaka, tukawapa tukipenda Mumwombe Mahuluka, faraja akawatenda Badala ya kutimuka, ili siku ya ulifi Hitaaihirishika, siku ya ndege kupanda Mkayajibu mashtaka, ya zenu ila...