Skip to main content

Bin-Adamu

Mimi
Natakadamu ino nudhumu
Nikayaambe yalomuhimu
Yanotaja ghilba za bin-Adamu
Wa kuhalalisha yalokharamu
kufaidi yake tamaa na hamumu
Yalo mema kayatiya sumu

Na
kuwaseta walomaamumu
Wakijigeuza sanamu
Wakisahau wali wanadamu
Kataka ibada kwa kaumu

Wadhani
Takwepa luhdi wakisha humu
Watakinza ya Mungu Kalamu
Kwamba Muhuluku hafahamu
ati hiyeyuki fuadi ngumu

Ila
Wendelepi siku ya hukumu?
Watapokwima mbele ya Hakimu
Kulipiya wao udhalimu
Kama si nyoto za Jehanamu?
Zitakao waunguza kwa zamu
Zikisha lamba mifupa na damu
Watauma zanda na kujilaumu
kwa wao utimamu wa wazimu

©Wamalwa

Comments

Popular posts from this blog

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Yupi mwenye haki

1.           Yupi ale mahuluki, asiye kuwa na doa Ni yupi ale na haki, asiye wa kukosoa Mja ambaye hakiuki, akawa wa kupotea Hayupo muenye haki, maki wote meondoa 2.           Yupi asiye wa kosa, mnyofu wazo nyendo, Awapo aseme sasa, akajinegee kando, Yule ale jitakasa, safi hanao uvundo Hakuna asiyekosa, kwa kauli na matendo 3.           Sijaona aliyejitosha, akahimili nafsiye Insi asejikunguisha, ulimi kwa kauliye Nani asiye keresha, kubughudhi muumbaye Ila tu akajikosha, akatubia dhambiye 4.           Nani asiyekunguwaa, kwa fikra ya moyoni Kunaye asiye na waa, lilofichama wazoni? Awe mja anayefaa, kwa Rabana machoni? Wote wamepunguwaa, utukufu hawaoni.   5.           Yupi basi wa kupona? amchaye Mola wake Nani ataka...