Skip to main content

Buriani swahiba

Siku pitile ayami, ukumbi sijasimama
Sijajitokea mimi, hata kauli kusema
Leo najiamba aimi, mbona sitasema lojema!
Niutunge na ulimi, n’nene ya yangu mtima

Kisema ni fika mimi, nimeipata naima
Mola ameshanihami, menikumbuka Karama
Kakomesha zangu kemi, kanondolea nakama
Ameshanipa mimi, wangu alo pa mtima

Ndio ukawa usemi, ninavyompenda Nelima
Nilitasema kwa semi, waja waje kusoma
Kuwa sina masghara mi’, nitampenda daima
Bure bure siungami, sivyo singesema

‘metujalia we nami, katupa nyota njema
Kajaazia na nyemi, na kila lililojema
Huba likasibu kumi,nyoyo zikafungama
Tupendane kwa ujumi, wala kwa nadama

Sa’ wakati mewadiya, wangu mimi kuhama
Nenda ughaibuniya, kwa mwaka huu mzima
Sivyo nivyodhaniya, kuwa mapenzi huuma
kawa tabu kwachaniya, japo  kweli ni lazima

Nomba hili nijuliya, nakuenzi kwa gharama
Hadi muhla wa kuuya, hubetu limesimama
Limefurikia ghaya, zaidi ya takadama
Kwa sasa buriani mbuya, ni mwiya wa kuchama

Hili nakuahidiya, kukupenda kwa daima
Nalo ninashikiliya, kwa nayo mawi na mema
indi  tu nitarejeya, hiyo yetu siku njema
Buriani wangu swahiya, Mola tujalie uzima

Hapa nakamiliya, mwisho n’tiye kaditama
Kama nivyosuhubiya, ndivyo hivyo daima
Nakutakia afiya, ya mwili nao mtima
Hadi twonane mbuya, n’kirejea na salama.












Comments

Popular posts from this blog

Hajafua Dafu Kama alivyo msasi, endaye kuwinda huwa Jenda kwa hamu na kasi,  kilenga kunasa njiwa Zimpatapo khasaisi, kumbe ndege hakutuwa Bado dafu hajafuwa, Mdavadi kijita Mesi Kwa makeke kahujuru, kuitafuta muruwa, Aionje hewa huru, kumbe nako  haikuwa Akapunjwa na Uhuru, alotaka kahiniwa Kabaki mechachamuwa,   zimwishiye furufuru Lisadiki sakumbimbi, walomlisha vongono  Kapotoshwa na wachimbi, na waja wasimaono Kamtowa kwenye kambi, alikopata usono Sasa yuasaga meno, akiulizwa haambi Kendea virambaramba, vichicha vya ukoloni Ndio navyo yuagamba, kuwa farasi mbioni Ni kama guo la mtumba, ‘pambwe mwari arusini Hata hawiki mjini, KANU jogoo wa shamba Nakoma wasiniambe, wanitusi wajuao Nachelea wanichimbe, wan’dhuru vibarakao Ila n’metowa ujumbe, wamwindhe nahodha wao “Sijetuwa meli yao, kwenye kaburi chimbe K.W Wamalwa Mlokole Mlumbi Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison

Ukila

Ukila kile kichakwe, cha mwenzio usile Ukila wa pupa ‘siwe, pupa nayo ni ndwele Ukila haramu s’tukue, cha mwendo sikitwale Ukila nla halali ‘we, cha chira na usile Usile waja kuamba, ‘kawa kauli nawe Usile ukajigamba, kukila kisichakwe Usile na kwa mafamba, litoe jasho lakwe Usile wala kuramba, na cha hila kisiliwe Kisiliwe cha litima, wasio na uwezo Kisiliwe cha yatima, chao wastahilizo Kisiliwe hata kama, wewe una uwezo Kisiliwe na cha umma, tatapika ulazo Ulazo na kwa ghiliba, huwa sumu mwenzangu, Ulazo na ukashiba, utalipa kwa Mungu Ulazo ziwezo baba, fedha za mwendo chungu Ulazo hata zi’haba, ziwe zako ndu’yangu

Mwana nakuasa

Leo nimekuita mwana, Nikupe yangu ya moyo Kwa upole nitanena ‘Kayatiye masikiyo Tabiya hii yako mwana Si yetu tujuwayo Uli wa kulaza damu Na uzembe uzidiyo Pahala nawe hudumu Uchao ni mbiyombiyo Hutufai nawe humu Na hiyo shambiroyo Wapendani naumi Unaiizia gange Hulimi na walimi Wataka ukajitenge Haya sijaona mimi Nakuasa ujichunge Mwiza kazi yu wa chira Ni aendewaye tenge Asiyetaka ajira Wala hashiki shilange Ndiye muja wa hasara Hubomoa asijenge Unavitaka vya bure Hulitoi jasho lako Lako ndizo hamrere Umebaki wa mitiko Uchao ‘wa’tuza bure Sizo zetu nyendo zako La mno lako ni ung’are Uzirembe nyele zako Uturi ujirashire Ukatembee kwa deko Hukosi kuzua ghere Na marashi ya mnuko Unazani utaoa? Utamwoa wa nani? Jasho nalo hujatoa, Utachokishika nini? Utaithibiti ndoa? Wa kukubali nani? Unafaa kujitoa, Fanye kazi kwa manani Na mali ukayazoa Hamadi kibindoni Ndipo utapopoa Ukamtafute mwendani Si mambo ya kutanga Fi na huyu fi na ...