Leo nimekuita mwana,
Nikupe yangu ya moyo
Kwa upole nitanena
‘Kayatiye masikiyo
Tabiya hii yako mwana
Si yetu tujuwayo
Uli wa kulaza damu
Na uzembe uzidiyo
Pahala nawe hudumu
Uchao ni mbiyombiyo
Hutufai nawe humu
Na hiyo shambiroyo
Wapendani naumi
Unaiizia gange
Hulimi na walimi
Wataka ukajitenge
Haya sijaona mimi
Nakuasa ujichunge
Mwiza kazi yu wa chira
Ni aendewaye tenge
Asiyetaka ajira
Wala hashiki shilange
Ndiye muja wa hasara
Hubomoa asijenge
Unavitaka vya bure
Hulitoi jasho lako
Lako ndizo hamrere
Umebaki wa mitiko
Uchao ‘wa’tuza bure
Sizo zetu nyendo zako
La mno lako ni ung’are
Uzirembe nyele zako
Uturi ujirashire
Ukatembee kwa deko
Hukosi kuzua ghere
Na marashi ya mnuko
Unazani utaoa?
Utamwoa wa nani?
Jasho nalo hujatoa,
Utachokishika nini?
Utaithibiti ndoa?
Wa kukubali nani?
Unafaa kujitoa,
Fanye kazi kwa manani
Na mali ukayazoa
Hamadi kibindoni
Ndipo utapopoa
Ukamtafute mwendani
Si mambo ya kutanga
Fi na huyu fi na yule
Chunga utajikaanga
Ati umetujile uwele
Mchumba chumbiya mwenga
Na yule ukamuole
Utafanyani kiwatunga,
Himila wakahimile
Na hilo likawe janga
Na lije likulemele
Mwanangu hutochenga
Wote wakikujile
Kisomo ndiyo unacho
Shahada umejitwaliya
Ujuzi unao kocho
Hutaki kuutumiya
Upate ukitakacho
Kile cha kukufaiya
Mwana wan’tiya kichocho
Kwona umejiachiya
Umekuwa kitumiwacho
Kidhani wawatumiya
Unawapa wapendacho
Nawanachokutakiya
Koma mwanangu ukome
Usinifishe mvyeleo
Usombombi uukome
Ukome kwanzia leo
Sitakwita te’niseme
Ishapita hii leo
Ukware si kuwa dume
Dume ni ajiwekeo
Wa sitaha ndiye dume
Anakheshimu nafseo
Muungwana kama kimeme
Fikiri nokwelezeo
Mradi unayo masikizi,
Haya umenisikiya
Kazituwe nyendo hizi
Ukawe wa kutuliya
Ukasuhubiye kazi
Halafu itakufaiya
Nakoma zaidi s’ezi
Yametosha mekwambiya
Nimekuweko na juzi
Miyaka menipitiya
Nimejizolea ujuzi
Ndiyo ya’ nakupa yaya
Comments