Skip to main content

Mwana nakuasa


Leo nimekuita mwana,
Nikupe yangu ya moyo
Kwa upole nitanena
‘Kayatiye masikiyo
Tabiya hii yako mwana
Si yetu tujuwayo

Uli wa kulaza damu
Na uzembe uzidiyo
Pahala nawe hudumu
Uchao ni mbiyombiyo
Hutufai nawe humu
Na hiyo shambiroyo

Wapendani naumi
Unaiizia gange
Hulimi na walimi
Wataka ukajitenge
Haya sijaona mimi
Nakuasa ujichunge

Mwiza kazi yu wa chira
Ni aendewaye tenge
Asiyetaka ajira
Wala hashiki shilange
Ndiye muja wa hasara
Hubomoa asijenge

Unavitaka vya bure
Hulitoi jasho lako
Lako ndizo hamrere
Umebaki wa mitiko
Uchao ‘wa’tuza bure
Sizo zetu nyendo zako

La mno lako ni ung’are
Uzirembe nyele zako
Uturi ujirashire
Ukatembee kwa deko
Hukosi kuzua ghere
Na marashi ya mnuko


Unazani utaoa?
Utamwoa wa nani?
Jasho nalo hujatoa,
Utachokishika nini?
Utaithibiti ndoa?
Wa kukubali nani?

Unafaa kujitoa,
Fanye kazi kwa manani
Na mali ukayazoa
Hamadi kibindoni
Ndipo utapopoa
Ukamtafute mwendani

Si mambo ya kutanga
Fi na huyu fi na yule
Chunga utajikaanga
Ati umetujile uwele
Mchumba chumbiya mwenga
Na yule ukamuole

Utafanyani kiwatunga,
Himila wakahimile
Na hilo likawe janga
Na lije likulemele
Mwanangu hutochenga
Wote wakikujile

Kisomo ndiyo unacho
Shahada umejitwaliya
Ujuzi unao kocho
Hutaki kuutumiya
Upate ukitakacho
Kile cha kukufaiya

Mwana wan’tiya kichocho
Kwona umejiachiya
Umekuwa kitumiwacho
Kidhani wawatumiya
Unawapa wapendacho
Nawanachokutakiya

Koma mwanangu ukome
Usinifishe mvyeleo
Usombombi uukome
Ukome kwanzia leo
Sitakwita te’niseme
Ishapita hii leo

Ukware si kuwa dume
Dume ni ajiwekeo
Wa sitaha ndiye dume
Anakheshimu nafseo
Muungwana kama kimeme
Fikiri nokwelezeo

Mradi unayo masikizi,
Haya umenisikiya
Kazituwe nyendo hizi
Ukawe wa kutuliya
Ukasuhubiye kazi
Halafu itakufaiya

Nakoma zaidi s’ezi
Yametosha mekwambiya
Nimekuweko na juzi
Miyaka menipitiya
Nimejizolea ujuzi
Ndiyo ya’ nakupa yaya

Comments

Popular posts from this blog

uketo wa sanaa ya ushairi

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda