Ukila kile kichakwe, cha mwenzio usile
Ukila wa pupa ‘siwe, pupa nayo ni ndwele
Ukila haramu s’tukue, cha mwendo sikitwale
Ukila nla halali ‘we, cha chira na usile
Usile waja kuamba, ‘kawa kauli nawe
Usile ukajigamba, kukila kisichakwe
Usile na kwa mafamba, litoe jasho lakwe
Usile wala kuramba, na cha hila kisiliwe
Kisiliwe cha litima, wasio na uwezo
Kisiliwe cha yatima, chao wastahilizo
Kisiliwe hata kama, wewe una uwezo
Kisiliwe na cha umma, tatapika ulazo
Ulazo na kwa ghiliba, huwa sumu mwenzangu,
Ulazo na ukashiba, utalipa kwa Mungu
Ulazo ziwezo baba, fedha za mwendo chungu
Ulazo hata zi’haba, ziwe zako ndu’yangu
Ukila wa pupa ‘siwe, pupa nayo ni ndwele
Ukila haramu s’tukue, cha mwendo sikitwale
Ukila nla halali ‘we, cha chira na usile
Usile waja kuamba, ‘kawa kauli nawe
Usile ukajigamba, kukila kisichakwe
Usile na kwa mafamba, litoe jasho lakwe
Usile wala kuramba, na cha hila kisiliwe
Kisiliwe cha litima, wasio na uwezo
Kisiliwe cha yatima, chao wastahilizo
Kisiliwe hata kama, wewe una uwezo
Kisiliwe na cha umma, tatapika ulazo
Ulazo na kwa ghiliba, huwa sumu mwenzangu,
Ulazo na ukashiba, utalipa kwa Mungu
Ulazo ziwezo baba, fedha za mwendo chungu
Ulazo hata zi’haba, ziwe zako ndu’yangu
Comments