Hajafua Dafu
Kama alivyo msasi, endaye kuwinda huwa
Jenda kwa hamu na kasi, kilenga
kunasa njiwa
Zimpatapo khasaisi, kumbe ndege hakutuwa
Bado dafu hajafuwa, Mdavadi kijita Mesi
Kwa makeke kahujuru, kuitafuta muruwa,
Aionje hewa huru, kumbe nako haikuwa
Akapunjwa na Uhuru, alotaka kahiniwa
Kabaki mechachamuwa, zimwishiye
furufuru
Lisadiki sakumbimbi, walomlisha vongono
Kapotoshwa na wachimbi, na waja
wasimaono
Kamtowa kwenye kambi, alikopata usono
Sasa yuasaga meno, akiulizwa haambi
Kendea virambaramba, vichicha vya ukoloni
Ndio navyo yuagamba, kuwa farasi mbioni
Ni kama guo la mtumba, ‘pambwe mwari arusini
Hata hawiki mjini, KANU jogoo wa shamba
Nakoma wasiniambe, wanitusi wajuao
Nachelea wanichimbe, wan’dhuru vibarakao
Ila n’metowa ujumbe, wamwindhe nahodha wao
“Sijetuwa meli yao, kwenye kaburi chimbe
K.W Wamalwa
Mlokole Mlumbi
Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison
Comments