Makonde ya usuhuba, hayo yanao wenyewe
Yanataka waloshiba, wakapandwa na viwewe
Aimi wa nguvuhaba! sezi viwavu n'waniwe
Huba ni la wa manguvu, n'lokifyefye najitowa
N'lokifyefye najitowa, niachiye wenye nguvu
Sitwai ningapawa, nachia yangu makovu
Kumbe hayanayo dawa, yenye kuleta utuvu
Vikumbo vyayo mapenzi, vyahitaji wenye navyo
Vyahitaji wenye navyo, wanotumia ja vyambo,
Ukicheza nao ovyo, hutohimili makumbo
Walai mja mimi sivyo, lau n'katowa matumbo
Masumbwi ya huba n'yao, wenye mbinu za mikono
Wenye mbinu za mikono, wajitenda pasi indha
Wajuzi wa mavongono, hini kwao ndio ladha
Kwazo kucha na vijino, wamewaatua kadha
Mafundo yayo mahaba, ni ya wale wasimoyo
Ni ya wale wasimoyo, walotasa wa hisia
Ndio walo na uchoyo, waja wanojitakia
Huwezi ngapiga mbio, au kilema takutia
Una kani chache flani, kana uwachie wao
Kana uwachie wao, nakwamba ni wachokozi
Kila kito ni cha kwao, sivyo wakulize chozi
Nawajua watu zao, mbwene na yangu maozi
Bahari’no ya mapenzi, ina papa wavumao
Ina papa wavumao, havipezi vikambare
Nashusha yangu matao, nepuke zao ndarire
Wanayo satua yao, ninawacha wasowere
Mikwato ya suhubani, ina hao masogora
Ina hao masogora, wasojuwa na hisani,
Ndio waja wenye chira, kupoka kwao ndo shani
Hawachi k’leta khasara, kuwatenga wendani
Hila zilo mapenzini, Walai zina wenyewe
Yanataka waloshiba, wakapandwa na viwewe
Aimi wa nguvuhaba! sezi viwavu n'waniwe
Huba ni la wa manguvu, n'lokifyefye najitowa
N'lokifyefye najitowa, niachiye wenye nguvu
Sitwai ningapawa, nachia yangu makovu
Kumbe hayanayo dawa, yenye kuleta utuvu
Vikumbo vyayo mapenzi, vyahitaji wenye navyo
Vyahitaji wenye navyo, wanotumia ja vyambo,
Ukicheza nao ovyo, hutohimili makumbo
Walai mja mimi sivyo, lau n'katowa matumbo
Masumbwi ya huba n'yao, wenye mbinu za mikono
Wenye mbinu za mikono, wajitenda pasi indha
Wajuzi wa mavongono, hini kwao ndio ladha
Kwazo kucha na vijino, wamewaatua kadha
Mafundo yayo mahaba, ni ya wale wasimoyo
Ni ya wale wasimoyo, walotasa wa hisia
Ndio walo na uchoyo, waja wanojitakia
Huwezi ngapiga mbio, au kilema takutia
Una kani chache flani, kana uwachie wao
Kana uwachie wao, nakwamba ni wachokozi
Kila kito ni cha kwao, sivyo wakulize chozi
Nawajua watu zao, mbwene na yangu maozi
Bahari’no ya mapenzi, ina papa wavumao
Ina papa wavumao, havipezi vikambare
Nashusha yangu matao, nepuke zao ndarire
Wanayo satua yao, ninawacha wasowere
Mikwato ya suhubani, ina hao masogora
Ina hao masogora, wasojuwa na hisani,
Ndio waja wenye chira, kupoka kwao ndo shani
Hawachi k’leta khasara, kuwatenga wendani
Hila zilo mapenzini, Walai zina wenyewe
Wamalwa K.W
Mlokole Mlumbi
Kamukuywa
Kamukuywa
Comments