Skip to main content

Buriani swahiba

Siku pitile ayami, ukumbi sijasimama
Sijajitokea mimi, hata kauli kusema
Leo najiamba aimi, mbona sitasema lojema!
Niutunge na ulimi, n’nene ya yangu mtima

Kisema ni fika mimi, nimeipata naima
Mola ameshanihami, menikumbuka Karama
Kakomesha zangu kemi, kanondolea nakama
Ameshanipa mimi, wangu alo pa mtima

Ndio ukawa usemi, ninavyompenda wa mtima
Nilitasema kwa semi, waja waje kusoma
Kuwa sina masghara mi’, nitampenda daima
Bure bure siungami, sivyo singesema

‘metujalia we nami, katupa nyota njema
Kajaazia na nyemi, na kila lililojema
Huba likasibu kumi,nyoyo zikafungama
Tupendane kwa ujumi, wala kwa nadama

Sa’ wakati mewadiya, wangu mimi kuhama
Nenda ughaibuniya, kwa mwaka huu mzima
Sivyo nivyodhaniya, kuwa mapenzi huuma
kawa tabu kwachaniya, japo kweli ni lazima

Nomba hili nijuliya, nakuenzi kwa gharama
Hadi muhla wa kuuya, hubetu limesimama
Limefurikia ghaya, zaidi ya takadama
Kwa sasa buriani mbuya, ni mwiya wa kuchama

Hili nakuahidiya, kukupenda kwa daima
Nalo ninashikiliya, kwa mawi na mema
Pindi tu nitarejeya, hiyo yetu siku njema
Buriani wangu mbuya, Mola atujaalie uzima

Comments

Popular posts from this blog

Bin-Adamu

Mimi Natakadamu ino nudhumu Nikayaambe yalomuhimu Yanotaja ghilba za bin-Adamu Wa kuhalalisha yalokharamu kufaidi yake tamaa na hamumu Yalo mema kayatiya sumu Na kuwaseta walomaamumu Wakijigeuza sanamu Wakisahau wali wanadamu Kataka ibada kwa kaumu Wadhani Takwepa luhdi wakisha humu Watakinza ya Mungu Kalamu Kwamba Muhuluku hafahamu ati hiyeyuki fuadi ngumu Ila Wendelepi siku ya hukumu? Watapokwima mbele ya Hakimu Kulipiya wao udhalimu Kama si nyoto za Jehanamu? Zitakao waunguza kwa zamu Zikisha lamba mifupa na damu Watauma zanda na kujilaumu kwa wao utimamu wa wazimu ©Wamalwa

Ukila

Ukila kile kichakwe, cha mwenzio usile Ukila wa pupa ‘siwe, pupa nayo ni ndwele Ukila haramu s’tukue, cha mwendo sikitwale Ukila nla halali ‘we, cha chira na usile Usile waja kuamba, ‘kawa kauli nawe Usile ukajigamba, kukila kisichakwe Usile na kwa mafamba, litoe jasho lakwe Usile wala kuramba, na cha hila kisiliwe Kisiliwe cha litima, wasio na uwezo Kisiliwe cha yatima, chao wastahilizo Kisiliwe hata kama, wewe una uwezo Kisiliwe na cha umma, tatapika ulazo Ulazo na kwa ghiliba, huwa sumu mwenzangu, Ulazo na ukashiba, utalipa kwa Mungu Ulazo ziwezo baba, fedha za mwendo chungu Ulazo hata zi’haba, ziwe zako ndu’yangu

Siku ya Ulifi

Toka Hegi yasikika, imelia parapanda Wafike walotajika, wasilimatie kwenda Majina waliandika, na ila walizotenda Waache kuhemeka, ili siku ya ulifi Nawaasa wahusika, waziache propaganda Hifai kulalamika, kila wanakokuenda Wengine tope kupaka, jukwaani wakipanda Wakuache kupayuka, ili siku ya ulifi Wenyewe waliyataka, mbegu mbaya walipanda Na chuki waliipika, ikaiva na kuvunda Na Umma ukagawika, maovu ukajitenda Sasa wana jakajaka, ili siku ya ulifi Mahuluki bila shaka, huvuna ‘lichopanda Na maji ukiyateka, uyanywe yote mafunda Na koo ikikabika, shauriyo ‘liyaenda Ela watawajibika, ili siku ya ulifi Wacheni kutikatika, kotekote mukiranda Mwakutaka kusifika, wafuasi mwawawinda Mwashinda kunung’unika, na mambo munayapinda Ishara ya kutishika, ili siku ya Ulifi Kama ni kutakasika, ni heri mkatuenenda Ghofira mkatutaka, tukawapa tukipenda Mumwombe Mahuluka, faraja akawatenda Badala ya kutimuka, ili siku ya ulifi Hitaaihirishika, siku ya ndege kupanda Mkayajibu mashtaka, ya zenu ila...