Skip to main content

Buriani swahiba

Siku pitile ayami, ukumbi sijasimama
Sijajitokea mimi, hata kauli kusema
Leo najiamba aimi, mbona sitasema lojema!
Niutunge na ulimi, n’nene ya yangu mtima

Kisema ni fika mimi, nimeipata naima
Mola ameshanihami, menikumbuka Karama
Kakomesha zangu kemi, kanondolea nakama
Ameshanipa mimi, wangu alo pa mtima

Ndio ukawa usemi, ninavyompenda wa mtima
Nilitasema kwa semi, waja waje kusoma
Kuwa sina masghara mi’, nitampenda daima
Bure bure siungami, sivyo singesema

‘metujalia we nami, katupa nyota njema
Kajaazia na nyemi, na kila lililojema
Huba likasibu kumi,nyoyo zikafungama
Tupendane kwa ujumi, wala kwa nadama

Sa’ wakati mewadiya, wangu mimi kuhama
Nenda ughaibuniya, kwa mwaka huu mzima
Sivyo nivyodhaniya, kuwa mapenzi huuma
kawa tabu kwachaniya, japo kweli ni lazima

Nomba hili nijuliya, nakuenzi kwa gharama
Hadi muhla wa kuuya, hubetu limesimama
Limefurikia ghaya, zaidi ya takadama
Kwa sasa buriani mbuya, ni mwiya wa kuchama

Hili nakuahidiya, kukupenda kwa daima
Nalo ninashikiliya, kwa mawi na mema
Pindi tu nitarejeya, hiyo yetu siku njema
Buriani wangu mbuya, Mola atujaalie uzima

Comments

Popular posts from this blog

uketo wa sanaa ya ushairi

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda