Skip to main content

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe
Si khiari asilani, rohoye aitowe
Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe
Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye

Ni kudura ya Manani, alompa utuwe
Hana na lake Fulani, sema akohowe
Hanalo la lakini, zake ziandikiwe
Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye        

Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe
Au aishi theneni, neema ajaliwe
Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe
Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye


Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye
Ngebaki duniani, amwali ajiliye
 Afurahi maishani, na wale wampendaye
Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Comments

Popular posts from this blog

uketo wa sanaa ya ushairi

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda