Skip to main content

Popular posts from this blog

Samehe usamehewe

Hayupo mja duniani asiyekosa asilani wala asitake samahani na imani ya mwenziwe Awe ndugu awe dada, au mwana.. Basi… kama hayupo asiyekosa akaitaka ghufira madhambiye kuondowa na , kwonewa imani na rehema, akawekwe huru nafsiye awe baba au mamaye binti au rafiki Basi, kwake kusahe ni faradhi mja mwene ila, samehe usamehewe Mlokole Mlumbi

uketo wa sanaa ya ushairi

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye