Wangu Laazizi
Ulivyojisabilia, kwangu pasi samahani,
Hujakosa kuniwia, radhi nili makosani,
na skomi kujivunia, kuwa nawe maishani
Mbuya wangu laazizi
Rahimu kanijalia, uwe wangu wa ubani,
kito nisichokilalia, kwangu ili hisani
Mola kaniumbia, uwe wangu muhisani,
Mbuya wangu laazizi
Mara nikikuwaza, nyemi hinija moyoni,
nafsi hukaramukia, ninapokutia
matoni
pamwe nawe sjajutia, wala nsaili kwa nini
Mbuya wangu laazizi
Na wajapotuchimbia, bado hatubandukani,
Mawi walotutakia, na tabu zilosakini
Yao hukuyasikia, ila uliniamini
Mbuya wangu laazizi
Mangapi umepitia, kunipenda maskini
Lufufu mevumilia, huba letu kudhamini
Vya mwiku umejilia, ukinipa na tumaini
Mbuya wangu laazizi!
Amwali hijitakia, ela uweja fulani
Wala raha kupania, kuishi utukufuni
Sakafu lijilalia, kusimisutu laini,
Mbuya wangu Laazizi!
Pukute ulijilia, hukukimwa majani
Sima ulibugia, mchana hata jioni
Chai kavu lijinywia, hukuuliza jibini
Mbuya wangu Laazizi!
Mlokole
Comments