Skip to main content

Wangu Laazizi!


Wangu Laazizi

Ulivyojisabilia, kwangu pasi samahani,

Hujakosa kuniwia, radhi nili makosani,

na skomi kujivunia, kuwa nawe maishani

Mbuya wangu laazizi

 
Rahimu kanijalia, uwe wangu wa ubani,

kito nisichokilalia, kwangu ili hisani

Mola kaniumbia, uwe wangu muhisani,

Mbuya wangu  laazizi


Mara nikikuwaza, nyemi hinija moyoni,

nafsi  hukaramukia, ninapokutia matoni

pamwe nawe sjajutia, wala nsaili kwa nini

Mbuya wangu laazizi

 
Na wajapotuchimbia, bado hatubandukani,

Mawi walotutakia, na tabu zilosakini

Yao hukuyasikia, ila uliniamini

Mbuya wangu laazizi


Mangapi umepitia, kunipenda maskini

Lufufu mevumilia, huba letu kudhamini

Vya mwiku umejilia, ukinipa na tumaini

Mbuya wangu laazizi!


Amwali hijitakia, ela uweja fulani

Wala raha kupania, kuishi utukufuni

Sakafu lijilalia, kusimisutu laini,

Mbuya wangu Laazizi!

 

Pukute ulijilia, hukukimwa majani

Sima ulibugia, mchana hata jioni

Chai kavu lijinywia, hukuuliza jibini

Mbuya wangu Laazizi!


Mlokole
 

 

Comments

Popular posts from this blog

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

mtu hafi kupenda

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

penzi

penzi la kulazimisha,lina gharama, kando na kukalifisha, linakukama, na linakufilisisha, likakukwama, hadi likakubakisha, u litima aimi nakujulisha, uwe salama usipende kujishasha, na kwa lazima penda anorejesha, nayo kheshima huba ja hili hukosha, wako mtima ... mbwene hoa walopenda, kwa kusukuma, hatimaye zao zanda, wakaziuma, kumbe hao walopenda, wamewahama amwalio zimeenda, sa' wamezama