Hayupo mja duniani
asiyekosa asilani
wala asitake samahani
na imani ya mwenziwe
Awe ndugu
awe dada,
au mwana..
Basi…
kama hayupo asiyekosa
akaitaka ghufira
madhambiye kuondowa
na ,
kwonewa imani
na rehema,
akawekwe huru nafsiye
awe baba
au mamaye
binti
au rafiki
Basi,
kwake kusahe ni faradhi
mja mwene ila,
samehe usamehewe
Mlokole Mlumbi
Comments