Skip to main content

Samehe usamehewe


Hayupo mja duniani
asiyekosa asilani
wala asitake samahani
na imani ya mwenziwe
Awe ndugu
awe dada,
au mwana..
Basi…
kama hayupo asiyekosa
akaitaka ghufira
madhambiye kuondowa
na ,
kwonewa imani
na rehema,
akawekwe huru nafsiye
awe baba
au mamaye
binti
au rafiki
Basi,
kwake kusahe ni faradhi
mja mwene ila,
samehe usamehewe


Mlokole Mlumbi

Comments

Popular posts from this blog

uketo wa sanaa ya ushairi

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye