Mimi
Natakadamu ino nudhumu
Nikayaambe yalomuhimu
Yanotaja ghilba za bin-Adamu
Wa kuhalalisha yalokharamu
kufaidi yake tamaa na hamumu
Yalo mema kayatiya sumu
Na
kuwaseta walomaamumu
Wakijigeuza sanamu
Wakisahau wali wanadamu
Kataka ibada kwa kaumu
Wadhani
Takwepa luhdi wakisha humu
Watakinza ya Mungu Kalamu
Kwamba Muhuluku hafahamu
ati hiyeyuki fuadi ngumu
Ila
Wendelepi siku ya hukumu?
Watapokwima mbele ya Hakimu
Kulipiya wao udhalimu
Kama si nyoto za Jehanamu?
Zitakao waunguza kwa zamu
Zikisha lamba mifupa na damu
Watauma zanda na kujilaumu
kwa wao utimamu wa wazimu
©Wamalwa
Natakadamu ino nudhumu
Nikayaambe yalomuhimu
Yanotaja ghilba za bin-Adamu
Wa kuhalalisha yalokharamu
kufaidi yake tamaa na hamumu
Yalo mema kayatiya sumu
Na
kuwaseta walomaamumu
Wakijigeuza sanamu
Wakisahau wali wanadamu
Kataka ibada kwa kaumu
Wadhani
Takwepa luhdi wakisha humu
Watakinza ya Mungu Kalamu
Kwamba Muhuluku hafahamu
ati hiyeyuki fuadi ngumu
Ila
Wendelepi siku ya hukumu?
Watapokwima mbele ya Hakimu
Kulipiya wao udhalimu
Kama si nyoto za Jehanamu?
Zitakao waunguza kwa zamu
Zikisha lamba mifupa na damu
Watauma zanda na kujilaumu
kwa wao utimamu wa wazimu
©Wamalwa
Comments