Skip to main content
Naja kwa jina lake Mungu
Kwamba yalo moyoni mwangu
Yaliyo tamu na machungu
Uje kulimuka mwenzangu
Ukituliana nikwambie

Nitasema pasi kificha
Nikuonye bila kukucha
Kuwa jambo ‘kikufikicha
La ukweli uliochacha
Nihisani uniambie

Hakuna aliyenyooka
Muenda asiyeteguka
Kwa wazo au kutamuka
Miye pia wakupunguka
Ukiona ila nambie

Ni wa chira asoonyeka
Muambae asokanyika
Mara tatu hajaambika
Atajuta akikutika
Zamu yako ni umwambie

Ukweli mchungu huuma
Na hugharimu kuusema
Ela ni dawa ya hatima
Huja kuuponya mtima
Ukiwa nao  we’nambie

Kanyo lako ukichelea
Ukiniona nakosea
Kwa Mungu ukijitetea
Hesabu utanitolea
Kujitoa ila,nambie

Niambie liwapo chungu
Usinifumbie mizungu
Walau likawe uchengu
Mwanga wa maozi yangu
Usiche kuindha nambie

Natua hapa nikuindha
Kwa hayo maonyo kadha
Kuyashika kwako faradha
Maishani yakupe ladha
Ela hikufai, nambie

©Wamalwa

Comments

Popular posts from this blog

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Yupi mwenye haki

1.           Yupi ale mahuluki, asiye kuwa na doa Ni yupi ale na haki, asiye wa kukosoa Mja ambaye hakiuki, akawa wa kupotea Hayupo muenye haki, maki wote meondoa 2.           Yupi asiye wa kosa, mnyofu wazo nyendo, Awapo aseme sasa, akajinegee kando, Yule ale jitakasa, safi hanao uvundo Hakuna asiyekosa, kwa kauli na matendo 3.           Sijaona aliyejitosha, akahimili nafsiye Insi asejikunguisha, ulimi kwa kauliye Nani asiye keresha, kubughudhi muumbaye Ila tu akajikosha, akatubia dhambiye 4.           Nani asiyekunguwaa, kwa fikra ya moyoni Kunaye asiye na waa, lilofichama wazoni? Awe mja anayefaa, kwa Rabana machoni? Wote wamepunguwaa, utukufu hawaoni.   5.           Yupi basi wa kupona? amchaye Mola wake Nani ataka...