Naja kwa jina lake Mungu
Kwamba yalo moyoni mwangu
Yaliyo tamu na machungu
Uje kulimuka mwenzangu
Ukituliana nikwambieNitasema pasi kificha
Nikuonye bila kukucha
Kuwa jambo ‘kikufikicha
La ukweli uliochacha
Nihisani uniambie
Hakuna aliyenyooka
Muenda asiyeteguka
Kwa wazo au kutamukaMiye pia wakupunguka
Ukiona ila nambie
Ni wa chira asoonyeka
Muambae asokanyika
Mara tatu hajaambika
Atajuta akikutika
Zamu yako ni umwambie
Ukweli mchungu huuma
Na hugharimu kuusemaEla ni dawa ya hatima
Huja kuuponya mtima
Ukiwa nao we’nambie
Kanyo lako ukichelea
Ukiniona nakosea
Kwa Mungu ukijitetea
Hesabu utanitolea
Kujitoa ila,nambie
Niambie liwapo chungu
Usinifumbie mizunguWalau likawe uchengu
Mwanga wa maozi yangu
Usiche kuindha nambie
Natua hapa nikuindha
Kwa hayo maonyo kadhaKuyashika kwako faradha
Maishani yakupe ladha
Ela hikufai, nambie
©Wamalwa
Comments