Skip to main content

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema
Ningepiga na kelele, ufahamu himahima
Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima
Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya

Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri
Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri
Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri
Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye

Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea
Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea
Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia
Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri

Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo
Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao
Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao
Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

Comments

Popular posts from this blog

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Yupi mwenye haki

1.           Yupi ale mahuluki, asiye kuwa na doa Ni yupi ale na haki, asiye wa kukosoa Mja ambaye hakiuki, akawa wa kupotea Hayupo muenye haki, maki wote meondoa 2.           Yupi asiye wa kosa, mnyofu wazo nyendo, Awapo aseme sasa, akajinegee kando, Yule ale jitakasa, safi hanao uvundo Hakuna asiyekosa, kwa kauli na matendo 3.           Sijaona aliyejitosha, akahimili nafsiye Insi asejikunguisha, ulimi kwa kauliye Nani asiye keresha, kubughudhi muumbaye Ila tu akajikosha, akatubia dhambiye 4.           Nani asiyekunguwaa, kwa fikra ya moyoni Kunaye asiye na waa, lilofichama wazoni? Awe mja anayefaa, kwa Rabana machoni? Wote wamepunguwaa, utukufu hawaoni.   5.           Yupi basi wa kupona? amchaye Mola wake Nani ataka...