Skip to main content

methali ya leo

Sipatwe n'kamba patwa n'gombe kula mpunga ngwa

Comments

Popular posts from this blog

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

mtu hafi kupenda

Mja hafi kupenda Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Mwana nakuasa

Leo nimekuita mwana, Nikupe yangu ya moyo Kwa upole nitanena ‘Kayatiye masikiyo Tabiya hii yako mwana Si yetu tujuwayo Uli wa kulaza damu Na uzembe uzidiyo Pahala nawe hudumu Uchao ni mbiyombiyo Hutufai nawe humu Na hiyo shambiroyo Wapendani naumi Unaiizia gange Hulimi na walimi Wataka ukajitenge Haya sijaona mimi Nakuasa ujichunge Mwiza kazi yu wa chira Ni aendewaye tenge Asiyetaka ajira Wala hashiki shilange Ndiye muja wa hasara Hubomoa asijenge Unavitaka vya bure Hulitoi jasho lako Lako ndizo hamrere Umebaki wa mitiko Uchao ‘wa’tuza bure Sizo zetu nyendo zako La mno lako ni ung’are Uzirembe nyele zako Uturi ujirashire Ukatembee kwa deko Hukosi kuzua ghere Na marashi ya mnuko Unazani utaoa? Utamwoa wa nani? Jasho nalo hujatoa, Utachokishika nini? Utaithibiti ndoa? Wa kukubali nani? Unafaa kujitoa, Fanye kazi kwa manani Na mali ukayazoa Hamadi kibindoni Ndipo utapopoa Ukamtafute mwendani S...