Skip to main content

Sipendi kucheka



Pana jambo ninatukiya, kwangu hilo ni muhali
Kitenda naona haya, kujishusha yangu hali
Stendi unipe hidaya sipendi kutenda hili
            Sipendi mimi kucheka

Sipendi mimi kucheka, kuchekea mawi
Sipendi na ya dhihaka, kwangu nyemi hiwi
Sipendi kwa hakika, mwovu kistawika
            Halafuye nikacheka!

Masikini akiteswa
Yatima akinyanyaswa
Mnyonge naye akinyonywa
Sipendi hata ikiwa
Unazonguvu najuwa
Na hili sitatekezwa

Mbona lakini nicheke, kwayo furaha?
Na wewe ukajiweke, uli na siha?
Na yatima ali pweke, wa anahaha?
Amenyimwa haki yake, hanayo raha!
Na moyo wangu ucheke, kwa ha,ha,ha!
Kucheka kwa kucheka
Mimi katu sitacheka

Comments

Popular posts from this blog

vingawa vyaliwa

Vingine kama kuliwa,vinono na vitamu Vinywewa au tafunwa,vinavyokutia hamu A cha hata ungapawa, viwavyo navyo haramu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, uindhari binadamu, Vingine havitaliwa, visikuletee hukumu Ulapo vikaliliwa, vitakugeuka sumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, punguza yako hamumu, Visiwe vinyang’anywa, gharama yake ni ngumu Vingapo hata kufichwa, kamwe navyo havidumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Vingine kama vyaliwa, vingine kwa utalamu, Vikawa havitambuwa, ashaona Mungu Karimu, Hakika vitatapikwa, peupe mbe’ ya kaumu Vitu vingawa vyaliwa, halali ndivyo muhimu Wamalwa Kevin Mlokole Mulumbi FLTA alumni 2010/2011

Mwana nakuasa

Leo nimekuita mwana, Nikupe yangu ya moyo Kwa upole nitanena ‘Kayatiye masikiyo Tabiya hii yako mwana Si yetu tujuwayo Uli wa kulaza damu Na uzembe uzidiyo Pahala nawe hudumu Uchao ni mbiyombiyo Hutufai nawe humu Na hiyo shambiroyo Wapendani naumi Unaiizia gange Hulimi na walimi Wataka ukajitenge Haya sijaona mimi Nakuasa ujichunge Mwiza kazi yu wa chira Ni aendewaye tenge Asiyetaka ajira Wala hashiki shilange Ndiye muja wa hasara Hubomoa asijenge Unavitaka vya bure Hulitoi jasho lako Lako ndizo hamrere Umebaki wa mitiko Uchao ‘wa’tuza bure Sizo zetu nyendo zako La mno lako ni ung’are Uzirembe nyele zako Uturi ujirashire Ukatembee kwa deko Hukosi kuzua ghere Na marashi ya mnuko Unazani utaoa? Utamwoa wa nani? Jasho nalo hujatoa, Utachokishika nini? Utaithibiti ndoa? Wa kukubali nani? Unafaa kujitoa, Fanye kazi kwa manani Na mali ukayazoa Hamadi kibindoni Ndipo utapopoa Ukamtafute mwendani S...