Skip to main content

mtu hafi kupenda

Mja hafi kupenda
Hapana mja duniani, apenda aondowe
Si khiari asilani, rohoye aitowe
Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe
Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye

Ni kudura ya Manani, alompa utuwe
Hana na lake Fulani, sema akohowe
Hanalo la lakini, zake ziandikiwe
Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye        

Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe
Au aishi theneni, neema ajaliwe
Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe
Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye

Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye
Ngebaki duniani, amwali ajiliye
 Afurahi maishani, na wale wampendaye
Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Comments

Popular posts from this blog

Ningekwambia!

Kama ingekuwa vile, swahiba ningeshasema Ningepiga na kelele, ufahamu himahima Kwamba sikuwazi miye, sikomi laili nzima Ningejasiri n’kwambie, lau sikupendi mbuya Kama sivyo ‘ngekwambiya, wazi wazi pasi siri Lau sijasuhubiya, nahari sikufikiri Kwamba sijakuwaziya, na gonezi kuabiri Ngaungama wangu mwari, kwamba siwe nimpendaye Kama kuli mwengineye, ninaye muenendea Mtimangu anitwaliye, ni radhi kumwenendea Hadhi yangu nimpaye, na siwe wangu maridia Ngakwambia siweye, hala ningekuhubiri Kama siwe ulinitwaa, kawa wa kunipa tuo Najenenda nili fwaa, nimetekwa na pumbao Azizi u’vyonivaa, yakaniisha matao Kweli ningeshakujuza, kwamba siwe nyonda

penzi

penzi la kulazimisha,lina gharama, kando na kukalifisha, linakukama, na linakufilisisha, likakukwama, hadi likakubakisha, u litima aimi nakujulisha, uwe salama usipende kujishasha, na kwa lazima penda anorejesha, nayo kheshima huba ja hili hukosha, wako mtima ... mbwene hoa walopenda, kwa kusukuma, hatimaye zao zanda, wakaziuma, kumbe hao walopenda, wamewahama amwalio zimeenda, sa' wamezama