Skip to main content

uketo wa sanaa ya ushairi

Mja hafi kupenda
Hapana mja duniani, apenda aondowe
Si khiari asilani, rohoye aitowe
Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe
Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye

Ni kudura ya Manani, alompa utuwe
Hana na lake Fulani, sema akohowe
Hanalo la lakini, zake ziandikiwe
Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye        

Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe
Au aishi theneni, neema ajaliwe
Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe
Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye


Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye
Ngebaki duniani, amwali ajiliye
 Afurahi maishani, na wale wampendaye
Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Comments

Popular posts from this blog

Bin-Adamu

Mimi Natakadamu ino nudhumu Nikayaambe yalomuhimu Yanotaja ghilba za bin-Adamu Wa kuhalalisha yalokharamu kufaidi yake tamaa na hamumu Yalo mema kayatiya sumu Na kuwaseta walomaamumu Wakijigeuza sanamu Wakisahau wali wanadamu Kataka ibada kwa kaumu Wadhani Takwepa luhdi wakisha humu Watakinza ya Mungu Kalamu Kwamba Muhuluku hafahamu ati hiyeyuki fuadi ngumu Ila Wendelepi siku ya hukumu? Watapokwima mbele ya Hakimu Kulipiya wao udhalimu Kama si nyoto za Jehanamu? Zitakao waunguza kwa zamu Zikisha lamba mifupa na damu Watauma zanda na kujilaumu kwa wao utimamu wa wazimu ©Wamalwa
Hajafua Dafu Kama alivyo msasi, endaye kuwinda huwa Jenda kwa hamu na kasi,  kilenga kunasa njiwa Zimpatapo khasaisi, kumbe ndege hakutuwa Bado dafu hajafuwa, Mdavadi kijita Mesi Kwa makeke kahujuru, kuitafuta muruwa, Aionje hewa huru, kumbe nako  haikuwa Akapunjwa na Uhuru, alotaka kahiniwa Kabaki mechachamuwa,   zimwishiye furufuru Lisadiki sakumbimbi, walomlisha vongono  Kapotoshwa na wachimbi, na waja wasimaono Kamtowa kwenye kambi, alikopata usono Sasa yuasaga meno, akiulizwa haambi Kendea virambaramba, vichicha vya ukoloni Ndio navyo yuagamba, kuwa farasi mbioni Ni kama guo la mtumba, ‘pambwe mwari arusini Hata hawiki mjini, KANU jogoo wa shamba Nakoma wasiniambe, wanitusi wajuao Nachelea wanichimbe, wan’dhuru vibarakao Ila n’metowa ujumbe, wamwindhe nahodha wao “Sijetuwa meli yao, kwenye kaburi chimbe K.W Wamalwa Mlokole Mlumbi Chuo Kikuu cha Wisconsin-Madison

Ukila

Ukila kile kichakwe, cha mwenzio usile Ukila wa pupa ‘siwe, pupa nayo ni ndwele Ukila haramu s’tukue, cha mwendo sikitwale Ukila nla halali ‘we, cha chira na usile Usile waja kuamba, ‘kawa kauli nawe Usile ukajigamba, kukila kisichakwe Usile na kwa mafamba, litoe jasho lakwe Usile wala kuramba, na cha hila kisiliwe Kisiliwe cha litima, wasio na uwezo Kisiliwe cha yatima, chao wastahilizo Kisiliwe hata kama, wewe una uwezo Kisiliwe na cha umma, tatapika ulazo Ulazo na kwa ghiliba, huwa sumu mwenzangu, Ulazo na ukashiba, utalipa kwa Mungu Ulazo ziwezo baba, fedha za mwendo chungu Ulazo hata zi’haba, ziwe zako ndu’yangu