Skip to main content

Tatasi za mtima


Kama unamjua jamani,
Kanisailie kwa nini
Mbona na mimi haneni,
na mwendoye sina sinani
Nachotaka ni hisani,
walahi sina kisirani
Nataka awe mwendani,
iwapo n'tapawa idhini

Zangu n’tetesi za mtima,
zan’tatiza hadi kusema
zanipa nyingi nakama,
na kupoka yangu naima
Anavyofanya si vyema,
kamuelezeni kwa hima
Kwamba ninaaengema,
na inaniisha neema

Kama ujumbe metuma,
ni kama kadinda kusoma
Kama sivyo angesema,
pengine naye akatuma
Kwa tuo ningesoma,
niyajue anayosema
Nijue kama ni kwema,
‘kajiamulie mapema

Nimeamba yote Nzisa,
sinayo mengine kwa sasa
lau kije kuwa kisa,
niliyemtaka nikakosa
Wala sinambe siasa,
ninaatilika kabisa
Ukimuona angusa,
na usiipoteze ruksa

Umwambie aitike,
si vyema akaniteleke,
Kwenye laini umweke,
ulainishe moyo wake
Macho yake afunguke,
na mtima wake uamke
Akubali miye wake,
aliye laazizi wake

N’ mema yenu maitiko,
ni heri kusema kuliko
Ila hayan’tui mtwiko,
wala yakanipa kiteko
Kan’tafutie aliko,
kamweleze hapa niliko
Sinacho mimi kicheko,
ni machozi ya mtiririko

Kweli hun’pati Rahabu,
unahitaji na hesabu
Kuyajua haya babu,
nimuambiayo habubu
Alejigeuza bubu,
hasikii wala hajibu
nafuu ja angejibu,
hata kwa ishara ni jibu

Haoni nivyostahabu,
na kungoja kama bawabu
Angaa nipate jibu,
jawabu litalonitibu,
H’jui kiburi harabu,
huua wala hakitibu
Hivyo mwambie sababu,
na kiini cha kunijibu

Comments

wamalwa said…
sanaa inaishi ati

Popular posts from this blog

Bin-Adamu

Mimi Natakadamu ino nudhumu Nikayaambe yalomuhimu Yanotaja ghilba za bin-Adamu Wa kuhalalisha yalokharamu kufaidi yake tamaa na hamumu Yalo mema kayatiya sumu Na kuwaseta walomaamumu Wakijigeuza sanamu Wakisahau wali wanadamu Kataka ibada kwa kaumu Wadhani Takwepa luhdi wakisha humu Watakinza ya Mungu Kalamu Kwamba Muhuluku hafahamu ati hiyeyuki fuadi ngumu Ila Wendelepi siku ya hukumu? Watapokwima mbele ya Hakimu Kulipiya wao udhalimu Kama si nyoto za Jehanamu? Zitakao waunguza kwa zamu Zikisha lamba mifupa na damu Watauma zanda na kujilaumu kwa wao utimamu wa wazimu ©Wamalwa

Ukila

Ukila kile kichakwe, cha mwenzio usile Ukila wa pupa ‘siwe, pupa nayo ni ndwele Ukila haramu s’tukue, cha mwendo sikitwale Ukila nla halali ‘we, cha chira na usile Usile waja kuamba, ‘kawa kauli nawe Usile ukajigamba, kukila kisichakwe Usile na kwa mafamba, litoe jasho lakwe Usile wala kuramba, na cha hila kisiliwe Kisiliwe cha litima, wasio na uwezo Kisiliwe cha yatima, chao wastahilizo Kisiliwe hata kama, wewe una uwezo Kisiliwe na cha umma, tatapika ulazo Ulazo na kwa ghiliba, huwa sumu mwenzangu, Ulazo na ukashiba, utalipa kwa Mungu Ulazo ziwezo baba, fedha za mwendo chungu Ulazo hata zi’haba, ziwe zako ndu’yangu

Kukrani!

Shukrani! Shukrani zangu jazila, kwa chama cha NCOLTCL (nikotiko) Akawajazi jaala, kwa kutupa mualiko Tumeteremea kulla, tulosoma toka kwako Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Sikomi kuwahongera, walimu walofundisha walivyojifunga nira, ya maarifa kutupasha Tuzijenge mbinu bora, Kiswahili kufundisha Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Mambo hayo ni muhimu, mlotupasha uchao Mliyeshusha magumu, ya nadharia zao Tuboreke walimu, kwa wale tufudnishao Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Hongera mwalimu Kiarie, kwa kuonyesha mifano Lisanza nikusifie, kwazo sifa nono nono Alwiya zikufikie, ulivyokuwa mfano Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Sikusahau Atonia, kwa wako ukakamavu, Jinsi ulokakania, pasi kuonya ochovu Uneemee dunia, kwa kutupa wangavu Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Wanafunzi mlofika, shukrani nyingi sana Kwenu kuwa washirika, na mwiya wenu kupana Na sisi tukazoeka, na vipindi vil...