Leo tamwona mwovu, amenawiri
Apataye kwa kiwavu,ndiye tajiri
Nawe uliye mnyovu, unayo shari
Chunga sikwingiye wivu, wewe subiri
Ajitendaye manguvu, na takaburi
Mchunguze vizuri
Kesho iatakudhihiri, ametoweka
Mtu yule aliyejibari, katononoka
Yamemkuta ya shari, ‘kaporomoka
Utafute kwa indhari, nayo hakika
Hutomwona nayo kheri, ameondoka
Mchunguze vizuri
Miye huyu nakweleze, yalo ya kweli
Zimefupishwa sikuze,haendi mbali
Mola ajua insize, k’watajamali
Ampa njema sikuze, mustakabali
Mwovu mali si malize, muhifadhili
Mchunguze vizuri
Asema wazi mwenyezi, kitabunimwe
Mjawe kumwacha hawezi, hatupwi kamwe
Waovu tawaweka wazi, shetani pamwe
Na wanyofu awajazi, wahifadhiwe
Wovu wadhili kwa kazi, wakufaidiwe
Mchunguze vizuri
Comments