Skip to main content

Tulikotoka!(limetafsiwa)

Huko tulikotoka!!
Japo hakuna umbo wala sura
Lakini kulituunda na kutupa sura
Japo wengi walilemazwa na kuachwa vichwara
Waliofahamu ngomani walisowera
Na umbali huu wajisukuma
Japo huenda kusizue tamaa
Na wengi waweza kupuuza
Lakini twakuonea fahari tunavyoweza
Tukijua  kumetupa na jina
Tulitoa machozi na bila raghba
Sasa twavuna naima tukiimba
Na hivyo tunamwadhimisha Yeye
Aliyetutia nguvu japo wanyonge tuwiliye
Sasa twakuonea fahari tulikotoka!!

Rejea, tazama na usailie
Utaona hakuna kitu ukifurahie
Na ukute kuwa hapana kitu kiwilie
Ulitima wake ulishamirie
Nusura kinamasini tuzamie
Lakini hatukutamauka tusishikilie
Kwa tumaini la ng’ambo litusubirie
Tukaipuuza njaa ilishadidie
Kwani nyoyo na nafsi zetu zilipanie
Wala zisitamauke na pale ziangukie.
Tumaini! Tumaini ndo nanga ilitushikilie
Tumaini la kesho itutadhayalie
….Na leo! Twatazama jana toka hapa tufikie
Twakutabasamia kwa fahari tulikotokea

Comments

Popular posts from this blog

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Yupi mwenye haki

1.           Yupi ale mahuluki, asiye kuwa na doa Ni yupi ale na haki, asiye wa kukosoa Mja ambaye hakiuki, akawa wa kupotea Hayupo muenye haki, maki wote meondoa 2.           Yupi asiye wa kosa, mnyofu wazo nyendo, Awapo aseme sasa, akajinegee kando, Yule ale jitakasa, safi hanao uvundo Hakuna asiyekosa, kwa kauli na matendo 3.           Sijaona aliyejitosha, akahimili nafsiye Insi asejikunguisha, ulimi kwa kauliye Nani asiye keresha, kubughudhi muumbaye Ila tu akajikosha, akatubia dhambiye 4.           Nani asiyekunguwaa, kwa fikra ya moyoni Kunaye asiye na waa, lilofichama wazoni? Awe mja anayefaa, kwa Rabana machoni? Wote wamepunguwaa, utukufu hawaoni.   5.           Yupi basi wa kupona? amchaye Mola wake Nani ataka...