Huko tulikotoka!!
Japo hakuna umbo wala sura
Lakini kulituunda na kutupa sura
Japo wengi walilemazwa na kuachwa vichwara
Waliofahamu ngomani walisowera
Na umbali huu wajisukuma
Japo huenda kusizue tamaa
Na wengi waweza kupuuza
Lakini twakuonea fahari tunavyoweza
Tukijua kumetupa na jina
Tulitoa machozi na bila raghba
Sasa twavuna naima tukiimba
Na hivyo tunamwadhimisha Yeye
Aliyetutia nguvu japo wanyonge tuwiliye
Sasa twakuonea fahari tulikotoka!!
Rejea, tazama na usailie
Utaona hakuna kitu ukifurahie
Na ukute kuwa hapana kitu kiwilie
Ulitima wake ulishamirie
Nusura kinamasini tuzamie
Lakini hatukutamauka tusishikilie
Kwa tumaini la ng’ambo litusubirie
Tukaipuuza njaa ilishadidie
Kwani nyoyo na nafsi zetu zilipanie
Wala zisitamauke na pale ziangukie.
Tumaini! Tumaini ndo nanga ilitushikilie
Tumaini la kesho itutadhayalie
….Na leo! Twatazama jana toka hapa tufikie
Twakutabasamia kwa fahari tulikotokea
Comments