Skip to main content

Ungejua wafu wamo!



Ugani ninajitoza, kilima mimi kulumba,
Angaa nikakujuza, nikakutoe ushamba,
Lau utajifunza, ili uwache kutamba,
Angejua wafu wamo, na humo kuna kaburi!

Washangaa nasemani,hebu nipe masikivu.
Nikudokolee  jamani, wewe usiye mtuvu,
Wendaye madanguroni, usiye saka wokovu,
Ungejua wafu wamo,na humo kuna kaburi!

Ngejizuia usare, utuwe uhayawani
Ukaukome ukware, ujituze na nyumbani,
Wewe si manoware, wakupenya machakani.
Ungejua wafu wamo, na humo mna kaburi!

Wengi huko wameenda, wakarejea na janga,
Labda hawakupenda! Uliwapeleka ujinga.
Sasa hivi wamekonda, majuto yanawatinga.
Ungejua wafu wamo, na humo muna kaburi!

 Humo muna kaburi, lisiloshibia tumbo,
Lawameza wa kiburi, walojaa jigambo,
 Walovaa takaburi, na kizitanua kumbo
Ugejua wafu wamo, na humo muna kaburi!

Ungeapa walahi, huko guulo hutii.
Moyowo ungenasihi, na kuomba kwa bidii,
Hata usije wahi, wala huko hupitii
Ungejua wafu wamo, na huko kuna kaburi.

Heri mie niondoke,lakini hili jitwalie.
Ukome na ukatike, katu usijililie
Utapobaki pweke ,yeyote asikujilie
Jangalo ulile peke, waja wamekuambaa!

Comments

Popular posts from this blog

Kukrani!

Shukrani! Shukrani zangu jazila, kwa chama cha NCOLTCL (nikotiko) Akawajazi jaala, kwa kutupa mualiko Tumeteremea kulla, tulosoma toka kwako Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Sikomi kuwahongera, walimu walofundisha walivyojifunga nira, ya maarifa kutupasha Tuzijenge mbinu bora, Kiswahili kufundisha Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Mambo hayo ni muhimu, mlotupasha uchao Mliyeshusha magumu, ya nadharia zao Tuboreke walimu, kwa wale tufudnishao Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Hongera mwalimu Kiarie, kwa kuonyesha mifano Lisanza nikusifie, kwazo sifa nono nono Alwiya zikufikie, ulivyokuwa mfano Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Sikusahau Atonia, kwa wako ukakamavu, Jinsi ulokakania, pasi kuonya ochovu Uneemee dunia, kwa kutupa wangavu Sasa tumeshalimuka, na mbinu za kufundisha Wanafunzi mlofika, shukrani nyingi sana Kwenu kuwa washirika, na mwiya wenu kupana Na sisi tukazoeka, na vipindi vil...

Siku ya Ulifi

Toka Hegi yasikika, imelia parapanda Wafike walotajika, wasilimatie kwenda Majina waliandika, na ila walizotenda Waache kuhemeka, ili siku ya ulifi Nawaasa wahusika, waziache propaganda Hifai kulalamika, kila wanakokuenda Wengine tope kupaka, jukwaani wakipanda Wakuache kupayuka, ili siku ya ulifi Wenyewe waliyataka, mbegu mbaya walipanda Na chuki waliipika, ikaiva na kuvunda Na Umma ukagawika, maovu ukajitenda Sasa wana jakajaka, ili siku ya ulifi Mahuluki bila shaka, huvuna ‘lichopanda Na maji ukiyateka, uyanywe yote mafunda Na koo ikikabika, shauriyo ‘liyaenda Ela watawajibika, ili siku ya ulifi Wacheni kutikatika, kotekote mukiranda Mwakutaka kusifika, wafuasi mwawawinda Mwashinda kunung’unika, na mambo munayapinda Ishara ya kutishika, ili siku ya Ulifi Kama ni kutakasika, ni heri mkatuenenda Ghofira mkatutaka, tukawapa tukipenda Mumwombe Mahuluka, faraja akawatenda Badala ya kutimuka, ili siku ya ulifi Hitaaihirishika, siku ya ndege kupanda Mkayajibu mashtaka, ya zenu ila...