Ugani ninajitoza, kilima mimi kulumba,
Angaa nikakujuza, nikakutoe ushamba,
Lau utajifunza, ili uwache kutamba,
Angejua wafu wamo, na humo kuna kaburi!
Washangaa nasemani,hebu nipe masikivu.
Nikudokolee jamani, wewe usiye mtuvu,
Wendaye madanguroni, usiye saka wokovu,
Ungejua wafu wamo,na humo kuna kaburi!
Ngejizuia usare, utuwe uhayawani
Ukaukome ukware, ujituze na nyumbani,
Wewe si manoware, wakupenya machakani.
Ungejua wafu wamo, na humo mna kaburi!
Wengi huko wameenda, wakarejea na janga,
Labda hawakupenda! Uliwapeleka ujinga.
Sasa hivi wamekonda, majuto yanawatinga.
Ungejua wafu wamo, na humo muna kaburi!
Humo muna kaburi, lisiloshibia tumbo,
Lawameza wa kiburi, walojaa jigambo,
Walovaa takaburi, na kizitanua kumbo
Ugejua wafu wamo, na humo muna kaburi!
Ungeapa walahi, huko guulo hutii.
Moyowo ungenasihi, na kuomba kwa bidii,
Hata usije wahi, wala huko hupitii
Ungejua wafu wamo, na huko kuna kaburi.
Heri mie niondoke,lakini hili jitwalie.
Ukome na ukatike, katu usijililie
Utapobaki pweke ,yeyote asikujilie
Jangalo ulile peke, waja wamekuambaa!
Comments