Skip to main content

Ungejua wafu wamo!



Ugani ninajitoza, kilima mimi kulumba,
Angaa nikakujuza, nikakutoe ushamba,
Lau utajifunza, ili uwache kutamba,
Angejua wafu wamo, na humo kuna kaburi!

Washangaa nasemani,hebu nipe masikivu.
Nikudokolee  jamani, wewe usiye mtuvu,
Wendaye madanguroni, usiye saka wokovu,
Ungejua wafu wamo,na humo kuna kaburi!

Ngejizuia usare, utuwe uhayawani
Ukaukome ukware, ujituze na nyumbani,
Wewe si manoware, wakupenya machakani.
Ungejua wafu wamo, na humo mna kaburi!

Wengi huko wameenda, wakarejea na janga,
Labda hawakupenda! Uliwapeleka ujinga.
Sasa hivi wamekonda, majuto yanawatinga.
Ungejua wafu wamo, na humo muna kaburi!

 Humo muna kaburi, lisiloshibia tumbo,
Lawameza wa kiburi, walojaa jigambo,
 Walovaa takaburi, na kizitanua kumbo
Ugejua wafu wamo, na humo muna kaburi!

Ungeapa walahi, huko guulo hutii.
Moyowo ungenasihi, na kuomba kwa bidii,
Hata usije wahi, wala huko hupitii
Ungejua wafu wamo, na huko kuna kaburi.

Heri mie niondoke,lakini hili jitwalie.
Ukome na ukatike, katu usijililie
Utapobaki pweke ,yeyote asikujilie
Jangalo ulile peke, waja wamekuambaa!

Comments

Popular posts from this blog

Mja hafi kupenda

Hapana mja duniani, apenda aondowe Si khiari asilani, rohoye aitowe Aingiye pa gizani, kusiko na mwendowe Maja hafi kupenda, n’ kudura itimiye Ni kudura ya Manani, alompa utuwe Hana na lake Fulani, sema akohowe Hanalo la lakini, zake ziandikiwe Mja hafi kupenda, n’kudura itimiye          Nyaka zikiwa shirini,ni jaala apawe Au aishi theneni, neema ajaliwe Mja hana kwa nini,ikiwa aitiwe Mja hafi kupenda,n’ kudura itimiye Lau ngapewa idhini, k’teuwa atakaye Ngebaki duniani, amwali ajiliye   Afurahi maishani, na wale wampendaye Mja hafi kupenda , n’kudura itimiye

Yupi mwenye haki

1.           Yupi ale mahuluki, asiye kuwa na doa Ni yupi ale na haki, asiye wa kukosoa Mja ambaye hakiuki, akawa wa kupotea Hayupo muenye haki, maki wote meondoa 2.           Yupi asiye wa kosa, mnyofu wazo nyendo, Awapo aseme sasa, akajinegee kando, Yule ale jitakasa, safi hanao uvundo Hakuna asiyekosa, kwa kauli na matendo 3.           Sijaona aliyejitosha, akahimili nafsiye Insi asejikunguisha, ulimi kwa kauliye Nani asiye keresha, kubughudhi muumbaye Ila tu akajikosha, akatubia dhambiye 4.           Nani asiyekunguwaa, kwa fikra ya moyoni Kunaye asiye na waa, lilofichama wazoni? Awe mja anayefaa, kwa Rabana machoni? Wote wamepunguwaa, utukufu hawaoni.   5.           Yupi basi wa kupona? amchaye Mola wake Nani ataka...