Nisikiye muandani, hili langu ‘takufaa
Likulinde maishani, upate na manufaa
Usikimbilie rahani, si kwote kwa shufaa
Raha siyo ya furaha, mbambonimwe mna karaha
Raha haiji kisolo, huja imepachana
Unalodhania silo, huwa limepindana
Unapolipata hilo, na jingine wakutana
Siirambitie raha, mbambonimwe mna karaha
Maumbile yakufunze, yana mfano murua
Kwanza mulima uanze, pindi bonde tagundua
Au mchana na nuruze, usiku utazipindua
Ukisha icheza zeze, simile kwaja simanzi
Husikii usesikiya, upate na uelewa
Wazee ‘lijisemeya, ja bakuli na kawa
Raha ukifurahiya, karaha hitachelewa
Mwana ukaindhari, baada ya raha karaha
Uchovyapo na asali, usiwe mwenye pupa sana
Na utamu wa asali, kuna nyuki na usena
Sasa uki si wa azali, una sumu ya usena
Na dunia k’ikumbata, kajikaliye yahiyatu
Tamati nimeifika, sina mengi ya kunena
Sipende kukaramka, ukakosa indhana
Raha simfanye kaka, rafiki wa kupendana
Mbona usena wa nyuki, nao huo si usena?
Comments